Friday, November 29, 2013

KINANA AUNGURUMA TUNDUMA

0 comments

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akihutumia maelfu ya wananchi katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mwaka, mjini Tunduma, wilayani Momba, jioni hii, Nov 28, 2013, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi na kuzungumza nao njia ya kuzitatua, katika mkoa wa Mbeya.
 Wananchi wakiwa wamembeba Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakati wa mkutano mkubwa wa hadhara uliohudhuria na maelfu ya wananchi katika uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya, leo
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye 'akihutoa dozi' alipohutubia katika mkubwa wa hadhara uliohudhuria na maelfu ya wananchi katika uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya, leo
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akitoa 'dozi' katika mkutano mkubwa wa hadhara uliohudhuria na maelfu ya wananchi katika uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya, leo
 Dk. Asha-Rose Migiro akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano uliofanyika  Uanja wa shule ya  Mwaka, Tunduma,leo
Katibu wa NEC, Siasa na Uhisiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (katikati mwenye  miwani) akiselebuka na wananchi kwenye mkutano, Uwanja wa shule ya  Mwaka, Tunduma leo. Imetayarishwa na theNkoromo Blog --

Endelea Kusoma >>
0 comments

Rais Dkt. Jakaya Kikwete apewa Uchifu wa Bariadi

D92A6333Mmoja wa machifu wa Kisukuma eneo la Bariadi ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki Andrew Chenge akimvika vazi la kijadi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kumpa uchifu Rais Kikwete iliyofanyika mjini Bariadi,Mkoa mpya wa Simiyu leo.Rais Kikwete alipewa jina la kisukuma la Chifu Ng’humbu Banhu lenye maana ya Anayekumbuka na kuthamini Watu. D92A6385Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amekalia kigoda cha Uchifu wa Bariadi baada ya kuwa Chifu Ng’humbu Banhu mjini Bariadi Mkoa mpya wa Simiyu leo.Rais Kikwete yupo katika Ziara ya Kikazi Mkoa mpya wa Simiyu(picha na Freddy Maro)
Endelea Kusoma >>

Thursday, November 28, 2013

0 comments

WAREMBO WAANZA KUJINOA TAYARI KWA SHINDANO LA MISS TANZANIA USA PAGEANT JUMAMOSI NOV 30



Lady Kate, Pamela, Ma Winny na Asha katika picha ya pamoja na Mamiss Tanzania USA.






Lady Kate mkurugenzi na mwanzilishi wa Miss Africa USA Pageant akiwaasa Mamiss Tanzania USA Pageant leo Jumamtano Novemba kwenye hotel ya Marriott
Pamela Egbe Messy mratibu wa Miss Africa USA Pageant akiwaelimisha walimbwende
MaWinny Casey Mkurugenzi na mwanzilishi wa Miss Tanzania USA Pageant katika picha ya pamoja na mratibu wa Miss Tanzania USA Pageant, Asha Nyang'anyi (kulia)
Mamiss Tanzania USA Pageant wakimsikiliza Lady Kate mkurugenzi na mwanzilishi wa Miss Africa USA Pageant alipokuwa. KUSOMA ZAIDI BOFYA READ MORE

*MTANZANIA CLARA NOOR AANZA KUNG'ARA MASHINDANO YA MISS EARTH UFILIPINO

 Mwandishi Wetu
Nyota wa mrembo wa Tanzania anayewania taji la Miss Earth, Clara Noor imeanza kung’ara baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika taji la fukwe ya Pagudpud iliyopo nchini Phillipines.
Mbali ya kutwaa taji hilo, Clara pia ameibuka mshindi wa tatu katika taji la vazi la Taifa na kuzipiku nchi nyingine nyingi na kuzawadiwa medali ya shaba.
Katika mashindano ya tuzo maalum, jumla ya tuzo 11 zilikuwa zinagombaniwa na warembo 88 walikuwa wanawania mataji hayo ambayo zawadi zake zilitolewa na wadhamini hao.
Clara alionyesha uwezo mkubwa katika taji hilo na kuwa mwafrika wa kwanza kushinda katika historia. Katika vazi la Taifa, Clara aliwavutia wengi na kupata ushindani mkubwa kutoka kwa mrembo wa warembo kutoka Afrika Kusini, Ashanti Mbanga na kutoka Nigeria, Marie Miller ambao walishika nafasi ya kwanza nay a pili.
Muandaaji wa Miss Earth Tanzania, Maria sarungi Tsehai alisema kuwa ni faraja kubwa kwa Clara kuitangaza Tanzania kwa kupitia mataji hayo mawili kwani mbali ya jina lake, kinachotangazwa pia ni nchi.
“Amefanya vyema mpaka sasa, tunatarajia kuona anaendelea kufanya vizuri na kutuletea sifa, mpaka sasa anastahili pongezi,” alisema Maria ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communications.
Alisema kuwa fainali ya mashindano hayo yatafanyika Desemba 7 kwenye ukumbi wa Versailles Palace, Alabang, Muntinlupa City na kurushwa live na vituo vya televisheni vya STAR World, ABS-CBN, Velvet, The Filipino Channel, Ustream na VenevisiĆ³n.

*MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA SHEREHE ZA MAADHIMISHO MIAKA 10 YA MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA (TCRA), DAR ES SALAAM.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi msaidizi Chumba cha Mtambo wa Kufuatilia Mawasiliano ya Simu (Telecommunicatins Traffic Monitoring System) Sunday Richard, wakati alipotembelea chumba hicho baada ya kufungua rasmi Sherehe za uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) leo katika ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof.Makame Mbarawa (wa pili kulia) ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Prof. John Nkoma. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hituba yake ya uzinduzi rasmi wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Miaka 10 ya Mapinduzi katika Sekta ya Mawasiliano Tanzania, yaliyozinduliwa rasmi leo katika Ukumbi wa Mliman City,jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Mawasiliano TCRA,akizungumza......
 Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof.Makame Mbarawa,akizungumza kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais.
 Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria ufunguzi huo....
 Baadhi ya wageni waalikwa na wadau wa mawasiliano wakiwa ukumbini humo....
 Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mawasiliano wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakijili meza kuu.
 Wadau.....
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Prof. John Nkoma, wakati alipotembelea katika chumba cha Mtambo wa Kufuatilia Mawasiliano ya Simu (Telecommunicatins Traffic Monitoring System) baada ya kufungua rasmi Sherehe za uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) leo katika ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof.Makame Mbarawa.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi msaidizi Chumba cha Mtambo wa Kufuatilia Mawasiliano ya Simu (Telecommunicatins Traffic Monitoring System) Sunday Richard, wakati alipotembelea chumba hicho baada ya kufungua rasmi Sherehe za uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) leo katika ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof.Makame Mbarawa (wa pili kulia) ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Prof. John Nkoma SUFIAN MAFOTO BLOG
Endelea Kusoma >>
0 comments

Tasnia ya Habari yapata pigo; Dunia mzobora hatunaye, kusikwa mchana huu

Dunia Mzobora enzi za uhai wake
TASNIA ya Habari imeendelea kupata mapengo baada ya Mwandishi  Mwandamizi wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo, Dunia Mzobora (49) kufariki dunia ghafla asubuhi ya jana wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokimbizwa kutoka Hospitali ya Aga Khan.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana zinasema kuwa, Mzobora aliyekuwa Kaimu Msanifu Mkuu wa gazeti la Uhuru, aliyewahi pia kuwa Naibu Mhariri wa Makala wa Mzalendo alifariki saa 12 asubuhi baada ya kuumwa ghafla usiku wa kuamkia jana akiwa nyumbani kwake.
Inaelezwa kuwa, mara baada ya kumaliza kulisimamia gazeti la Uhuru toleo la jana (Jumatano), hali yake ilibadilika na kulazimisha ndugu zake kumkimbiza hospitali ya Aga Khan, lakini hali ilizidi kuwa mbaya na kuwahishwa Muhimbili na wakati madaktari wakiendelea kuokoa maisha yake aliaga dunia.
Marehemu Mzobora, aliyezaliwa April 6, 1964 Mwandege mkoani Kigoma anatarajiwa kuzikwa mchana huu katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.
Binafsi niliwahi kufanya kazi na Mzobora enzi za uhai wake wakati nafanya kazi Uhuru/Mzalendo na alikuwa ni mchapakazi, mcheshi na mwanamichezo.
Licha ya ucheshi, lakini marehemu Mzobora alikuwa makini katika kazi yake na alikuwa mmoja wa 'mabosi' wangu waliokuwa wakipenda kwa kujiweka watanashati karibu muda wote kiasi kilikuwa napenda kumuita 'Papaa'.
Mungu aiweke mahali pema roho ya marehemu Dunia Mzobora, yeye katangulia nasi tu nyuma yake na MICHARAZO inaungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu kwa kuwataka wawe na subira.
Endelea Kusoma >>

Wednesday, November 27, 2013

0 comments

SELCOM,VODA COM NA OIL COM WAUNGANA KURAHISISHA UNUNUZI WA MAFUTA KWA NJIA YA MPESA




Meneja wa huduma za Selcom,Bi,Everline Simpilu kushoto akitoa lisiti kwa mteja  wa mafuta wa kituo cha Oil Com Bw,Peter Ibrahimu wakati wa uzinduzi wa ununuaji wa mafuta kwa njia ya mtandao wengine wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Oil Com Bw,Mohamed Said Nahdi Ofisa wa Selcom Tumaini Mgori na Meneja husiano wa nje wa kampuni ya Vodacom Salumu Mwalimu huduma za kununua mafuta kwa njia ya mtandao zitakuwa zikitolewa na kampuni ya vodacom kupitia Mpesa ambapo uzinduzi huo ulifanyika Dar es salaam jana Kampuni ya Selcom ndio wawezeshaji na mashine zao  za POS ndio zitakazokuwa zikitumika picha na Mpiga picha  wetu

Meneja wa huduma za Selcom,Bi,Everline Simpilu kushoto akimpatia lisiti kwa mteja  wa mafuta wa kituo cha Oilcom Bw,Peter Ibrahimu wakati wa uzinduzi wa ununuaji wa mafuta kwa njia ya mtandao wengine wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Oilcom Bw,Mohamed Said Nahdi Ofisa wa Selcom Tumaini Mgori na Meneja husiano wa nje wa kampuni ya Vodacom Salumu Mwalimu huduma za kununua mafuta kwa njia ya mtandao zitakuwa zikitolewa na kampuni ya voda com kupitia Mpesa na mashine pekee za Selcom POS  uzinduzi huo ulifanyika Dar es salaam jana picha na Mpiga picha  wetu

Meneja wa huduma za Selcom,Bi,Everline Simpilu kushoto  akimweleza mwendesha bajaji Bw,Peter Ibrahimu  jinsi Selcom wanavyotoa huduma ya kununua mafuta kwa njia ya mtandao kwa kushirikiana na ,Vodacom Mpesa katika huduma ya lipa bidhaa pamoja na Oil Com

Meneja wa huduma za Selcom,Bi,Everline Simpilu kushoto Group IT meneja  wa Oil Com, Abubakari Mwita,Mkurugenzi wa Oil Com Bw,Mohamed Said Nahdi, Meneja husiano wa nje wa kampuni ya Vodacom Salumu Mwalimu.Ofisa wa Selcom Tumaini Mgori wakipata maelezo jinsi mashine ya Selcom inavyofanya kazi ya kununua mafuta kwa njia ya mtandao wakiungana na Oilcom na Vodacom  kupitia huduma ya lipa bidhaa  wakati wa uzinduzi uliyofanyika Dar es salaam jana picha na Mpiga picha  wetu
Ofisa wa Selcom Tumaini Mgori akiongea na wahandishi wa habari wakati wa huzinduzi wa huduma hiyo
Endelea Kusoma >>
0 comments

 NA       BONIFACE WAMBURA
MECHI YA TANZANITE SASA KUCHEZWA DAR
Mechi ya kwanza ya raundi ya michuano ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kwa wanawake chini ya miaka 20 kati ya Tanzania (Tanzanite) na Afrika Kusini iliyokuwa ichezwe Mwanza sasa itafanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Baada ya ukaguzi uliofanywa na maofisa wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imebainika uwanja huo unatakiwa ufanyiwe marekebisho ambayo hayawezi kuwahi Desemba 7 mwaka huu, siku ambayo ndiyo mechi hiyo inatakiwa kuchezwa.

Vyumba vya wachezaji vya uwanja huo ndilo eneo ambalo linatakiwa  kufanyiwa marekebisho makubwa.

KILIMANJARO STARS YATUA SALAMA NAIROBI
Timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) imewasili salama Nairobi, Kenya tayari kwa mashindano ya Kombe la Chalenji yanayoanza kesho (Novemba 27 mwaka huu) katika Uwanja wa Nyayo.

Kilimanjaro Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iliwasili saa 3 usiku kwa ndege ya RwandAir, na imefikia katika hoteli ya Sandton iliyoko katikati ya Jiji la Nairobi.

Kwa mujibu wa programu ya Kocha Mkuu Kim Poulsen, Kilimanjaro Stars leo (Novemba 26 mwaka huu) ni mapumziko ambapo kesho itafanya mazoezi kujiandaa kwa mechi yake ya kwanza dhidi ya Zambia itakayochezwa Novemba 28 mwaka huu Uwanja wa Machakos.

WANNE WASHINDA UCHAGUZI CECAFA
Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limepata wajumbe wapya wa wanne wa Kamati ya Utendaji katika uchaguzi uliofanya leo (Novemba 26 mwaka huu) hoteli ya Hillpark jijini Nairobi.
Uchaguzi huo ulifuatiwa na Mkutano Mkuu wa CECAFA ulioongozwa na Mwenyekiti wake Leodegar Tenga na kuhudhuriwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Kalusha Bwalya na ofisa wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Emmanuel Maradas.

Rais wa zamani wa Shirikisho la Vyama vya Mpira wa Miguu Uganda (FUFA), Lawrence Mulindwa ndiye aliyeongoza katika uchaguzi huo ambapo wasimamizi walikuwa Bwalya na Maradas.

Mulindwa alipata kura zote 12 na kufuatiwa na Tariq Atta wa Sudan (10), Abdigaani Saeb Arab wa Somalia (9) na Raoul Gisanura wa Rwanda (8). Atta, Arab na Gisanura walikuwa wakitetea nafasi zao.

Walioshindwa ni Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Sudan Kusini (SSFA), Alei Chabor aliyepata kura tano na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kenya (FKF), Sam Nyamweya aliyepata kura nne.

MICHUANO YA UHAI YAHAMIA CHAMAZI
Michuano ya Kombe la Uhai imeingia hatua ya robo fainali ambapo sasa mechi zinachezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Uamuzi wa kuhamisha mechi hizo kutoka viwanja vya Karume na DUCE ni kuziwezesha zote kuoneshwa moja kwa moja (live) na Azam Tv.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tunaomba radhi kwa washabiki ambao watakuwa wameathirika kutokana na uamuzi huo.

USAJILI DIRISHA DOGO KUFUNGWA DESEMBA 15
Wakati dirisha dogo la usajili linafungwa Desemba 15 mwaka huu, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tunazikumbusha klabu zote kuheshimu kanuni na kuzingatia muda uliowekwa.

Pia tunakumbusha kuwa kupeleka mchezaji kwa mkopo katika klabu nyingine hakutoi nafasi ya kusajili mchezaji mpya. Kama klabu ilisaji wachezaji 30 maana yake ni kuwa haina nafasi ya kuongeza wachezaji.

Kwa upande wa wachezaji wa kigeni (foreign players), tunakumbusha kuwa kuanzia msimu ujao 2014/2015 watakuwa watatu tu badala ya watano wa sasa.

Kuhusu usajili wa wachezaji kutoka nje mpaka sasa hakuna hata klabu moja imeshaingia kwenye TMS kuomba uhamisho. Itakapofika Desemba 15, system ya TMS itafunga.
RAMBIRAMBI MSIMBA WA ANDREW KILOYI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mwamuzi wa zamani wa FIFA, Andrew Kiloyi kilichotokea mjini Iringa.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mahano, Kiloyi alifariki dunia juzi (Novemba 24 mwaka huu) kutoka na ugonjwa wa fangasi ya ubongo, na marehemu amesafirishwa kwenda kwao Kigoma ambapo atazikwa.

Kiloyi alizaliwa Mei 5, 1968. Alijiunga na uamuzi wa mpira wa miguu mwaka 1988 ambapo alipata beji ya FIFA mwaka 2001 akiwa mwamuzi msaidizi. Alistaafu uamuzi mwaka 2009, na hadi anafariki akiwa mjumbe wa Kamati ya Waamuzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Iringa (IREFA).

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pole kwa familia ya marehemu, IREFA, ndugu, jamaa na marafiki kutokana na msiba huo na kuwataka kuwa na moyo wa subira na uvumilivu katika kipindi hicho cha majonzi. Mungu aiweka mahali pema roho ya marehemu Kiloyi.  

Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Endelea Kusoma >>
0 comments


MAKADA CHADEMA JIMBO LA IRINGA MJINI WAJIUNGA CCM ,WAMPIGA MAKOMBORA MAZITO MBUNGE MCHUNGAJI MSIGWA


 
 Mwenyekiti  wa CCM mkoa wa Iringa  Jesca Msambatavangu  akiwapokea  makada wa Chadema jimbo la Iringa mjini  walioamua  kuachana na Chadema na kujiunga na CCM
 Maandamano  ya  boda boda na magari  katika  kuhitimisha  mbio za Bendera  ya  CCM mkoa  wa Iringa
 Wananchi  wa maeneo ya  Miyomboni  eneo la mashine  tatu  wakishuhudia msafara wa Bendera  ya  CCM  ukipita  eneo hilo
 Makada wa Chadema  wakisalimisha kadi zao kwa mwenyekiti wa CCM mkoa  wa Iringa Bi Jesca Msambatavangu
 Umati  mkubwa wa  wananchi waliojipanga  barabarani  wakati  wa msafara  wa bendera  ukipita
 Msafara  wa bendera  katika  manispaa ya  Iringa
 Wananchi  wakiwa katika mkutano  wa  kilele  cha mbio za bendera  mkoa  wa Iringa

 Vijana  walioshiriki  kukimbiza  bendera ya CCM mkoa  wa Iringa
Kada  wa  Chadema katikati Violeth Mwakisyala akiwa ameungana na wana CCM kuweka alama ya dole baada ya  kujivua Chadema na  kujiunga CCM
Kada wa CCM Bw  Julio Elieza kushoto akisoma maandishi ya CHANA GWANDA NA GAMBA NA  VAA UZALENDO mara  baada ya kujiunga na CCM akitokea Chadema
 kada  wa Chadema  Bw Mmasi akionyesha kadi  yake ya  Chadema kabla ya kujiunga na  CCM katika  kilele  cha mbio  za bendera
 Mwenyekiti  wa  CCM mkoa wa Iringa  akimkaribisha  CCM Bi Violeth  baada ya  kujiengua  Chadema


 Makada  na  wapiganaji  wa Chadema  waliojiunga na CCM
 Kiapo cha  utii  kwa  waliojiunga na CCM kutoka  vyama  mbali mbali
 Kiongozi  mkuu wa mbio  za bendera  Alli  Simba akijiandaa kumkabidhi  bendera diwani  wa kata  ya Makorongoni Bw Thadeus Tenga  ili akabidhi kwa  mwenyekiti  wa CCM mkoa
 Tenga  akijiandaa kupokea  bendera  toka kwa Simba
 Mwenyekiti wa CCM mkoa  wa Iringa  Jesca Msambatavangu kulia akipokea  bendera  toka kwa diwani wa kata ya makorongoni na kiongozi wa  mbio hizo
Na  Francis Godwin BLog,Iringa

MBUNGE wa jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amerushiwa makombora na baadhi ya wanachama wa chama hicho ambao juzi walitimkia Chama cha Mapinduzi (CCM).

 
Makombora hayo yalirushwa katika uwanja wa Mwembetogwa mjini hapa, wakati CCM Mkoa wa Iringa ikihitimisha mbio zake za bendera ya CCM.
 
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu  alisema lengo la mbio za bendera ya CCM ni kuhamasisha amani na utulivu nchini.
 
Malengo mengine ni kukagua utekelezaji wa Ilani ya chama hicho unaofanywa na serikali, kuhamsisha vijana kujiajiri na kuwashukuru watanzania kwa kuendelea kuinga mkono CCM.
 
Katibu Uenezi na Itikadi Mkoa wa Iringa, Dk Yahaya Msigwa alisema jumla ya wanachama 120 kutoka vyama mbalimbali vya upinzani kikiwemo Chadema wamerejea CCM kupitia mbio hizo.
 
Baadhi ya wanachama wa Chadema waliokabidhiwa kadi zao kwenye hitimisho la mbio hizo zilizoanza miezi miwili iliyopota ni pamoja na Ibrahim Mmasi na Vaileti Mwakisyala.
Akirusha makombora kwa Mchungaji Msigwa, Mmasi alisema ni kiongozi asiyeambilika huku akimtuhumu kwamba ni mroho wa madaraka .
 
Mmasi alisema wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2010, Mchungaji Msigwa aliwatuhumu baadhi ya viongozi akiwemo aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Monica Mbega (CCM) kwa kuwa na vyeo vingi vya kisiasa hali iliyosababisha ashindwe kutekeleza wajibu wake kwa wananchi.
 
“Wananchi walimsikia Mchungaji Msigwa na kumpa ubunge, lakini baada ya kupata nafasi hiyo anazidi kujilimbikizia vyeo hali inayofinya demokrasia ndani ya chama,” alisema.
 
Akivitaja baadhi ya vyeo vya mbunge huyo, Mmasi alisema mbali ya kuwa mbunge, Mchungaji huyo ni diwani, mwenyekiti wa chama hicho wilaya, mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na waziri kivuli.
 
Alisema hali ya kisiasa ndani ya chama hicho wilayani hapa na mkoani kwa ujumla sio nzuri kwa kuwa hakuna demokrasia ya kukosoa na kukosolewa.
 
“Kuna udikteta wa mawazo, watu wakisema ukweli wanachukiwa, mambo hayako shwari hata kidogo,” alisema.
 
Alisema kuna viongozi ambao hawapikiki chungu kimoja na mchungaji Msigwa, hawasalimiani, hawaaminiani kwa kile kinachoelezwa kwamba hapendi kukosolewa.
 
Huku akishangiliwa na baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo, Mmasi alisema kabla ya Uchaguzi Mkuu ujao, Chadema mjini Iringa itakuwa imesambaratika.
 
“Uchaguzi ndani ya chama hicho umekaribia, waliopo na tuliokuwepo tunajua kinachoendela, hali sio nzuri kwasababu wanachama walio wengi wanataka mabadiliko, hali hiyo haitawaacha salama,” alisema.
 
 huku   wanachama   zaidi  ya 200 wapya  wakijiunga na  chama  hicho  huku  baada ya  makada  wa chama  cha  Demokrsani na maendeleo (CHADEMA)  wakijiengua katika chama  hicho na kujiunga na CCM.
Makada  hao  wa Chadema  wameeleza  kufurahishwa na utendaji kazi wa serikali ya CCM na kuchukizwa  kile  walichodai ni ubabaishaji wa Chadema katika ngani ya jimbo , mkoa  na Taifa kwa madai  kuwa  vitendo vya kifisadi  ndani ya Chadema  ni moja ya  sababu ya  wao  kujiengua.
Makada  hao wakitumia  muda  mwingi kushambulia  mbunge  wa jimbo la Iringa mjini na  diwani  wa Mvinjeni  na viongozi  wa Chadema  taifa  walisema  kuwa  wamechoshwa na porojo za  viongozi  hao. 
Pia  vijana  hao  walisema  kuwa  wamekuwa wakipokea  vitisho  mbali mbali kutoka kwa  viongozi na makada wa Chadema  pale wanapotaka  kuhamia CCM
   
Msambatgavangu  alisema  kuwa  CCM  mkoa  wa  Iringa  haitawavumilia   viongozi  wa serikali  ambao watashindwa  kutekeleza majukumu yao .
Huku  ikiwatoa  hofu vijana  waliopo upinzani ambao  wanataka  kurudi CCM kuwa  wana uhuru wa kwenda  chama chochote cha  siasa.
 
Kwa kupitia mbio hizo za bendera Msambatavangu alisema jumla ya wanachama wapya 4,000 wamepatikana katika wilaya zote za mkoa wa Iringa, na wanachama zaidi ya 1,000 wamejiunga na jumuiya mbalimbali za CCM


On Wednesday, November 27, 2013 12:32 AM, Bashir Nkoromo <nkoromo@gmail.com> wrote:
CAPTIONS
1. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Ujumbe wake (katikati) wakiwa wamezungukwa na umati wa wananchi, Kinana alipokuwa akizindua Shina la Wakereketwa Wajasirimali wa Kikundi cha Amani na Maendeleo cha waendesha bodaboda, Katika Kata ya Kiwira, Rungwe mkoani Mbeya, Nov 27, 2013.

2. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi  nyumba ya mwalimu katika shule ya sekondari Kaya ya Ikuti, wilayani Rungwe mkoani Mbeya, Nov 27, 2013.

3. Wananchi katika Kata ya Ikuti, wilayani Rungwe wakimshangilia Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana (Hayupo Pichani) huku wengine wakiwa juu ya miti ili kumuona kiongozi huyo wa CCM, katika mkutano wa hadhara, uliofanyika Nov 27, 2013, katika kata hiyo.

4. Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, akihutubia wananchi wa Kata ya Masoko, Rungwe, mkoani Mbeya, Nov 27, 2013.

5. Katibu wa NEC, Itikasi na Uenezi, Nape Nnauye akifurahia jambo na Mbunge wa Rungwe Magharibi,Prof. David Mwakyusa, wakati wa mkutano uliofanyika katika jimbo hilo, Kata ya Masoko, wilayani Rungwe mkoani Mbeya, Nov 27, 2013.

5b.Katibu wa NEC, Itikasi na Uenezi, Nape Nnauye akimkumbatia kwa furaha Mbunge wa Rungwe Magharibi, Prof. David Mwakyusa, wakati wa mkutano uliofanyika katika jimbo hilo, Kata ya Masoko, wilayani Rungwe mkoani Mbeya, Nov 27, 2013

6. Wananchi waliokuwa wakifanya biashara katika soko la Kata ya Ikuti, katika kijiji cha Butonga, wilayani, Rungwe, wakiwa wameacha biashara zao na kuzuia msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana ili kumweleza kero zao, alipokuwa akipita eneo hilo, akiwa katika ziara ya kukagua utelezaji ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi na kujaliana nao njia bora ya kuzitatua, Nov 27, 2013.

7. Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akipewa zawadi na Jane James, Mke wa Mjumbe wa Shina namba 2, Butonga, Kata ya Ikuti, Rungwe, James Mbasi, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alipotembelea nyumbani kwa mjumbe huyo, Nov 27, 2013.

8. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpongeza kijana  Asimwise mwantebele baada ya kijana huyo kutangaza kuhamia CCM akitokea Chadema, wakati Katibu Mkuu huyo alipokuwa akizindua shina la wakereketwa wa CCM la Kiwira, wilayani Rungwe, Nov 27, 2013.

9. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimhoji jukwaani, Mkuu wa wilaya ya Rungwe, Crispian Meela (kushoto) ni kwa kiwango gani amesimamia utekelezaji wa ilani ya CCM, wilayani kwake, wakati wa mkutano wa hadhara kata ya Ikuti, wilayani humo, mkoani Mbeya, Nov 27, 2013.

10. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na inamama wauza ndizi wa  Iponjola, wilayani Rungwe mkoaoni Mbeya, Nov 27, 2013.
Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu