Saturday, August 31, 2013

0 comments

SHULE YAWAZUIA ROBO TATU YA WANANFUNZI WAKE KUFANYA MITIHANI SHINYANGA, KISA MICHANGO!!

SHINYANGA, Tanzania 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida robo tatu ya wanafunzi katika shule ya sekondari Uhuru iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga wamezuiwa kufanya mitihani ya muhula wa pili kwa madai ya wazazi wao kushindwa kulipia michango mbalimbali.

Baadhi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo waliozungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa walisema pamoja na kuzuiwa kufanya mitihani hiyo walimu wao waliwapa adhabu ya kukaa chini wakiwa juani na baadae walipewa kazi ya kumwagilia bustani wakati wenzao wachache wakiendelea na mitihani.

Mmoja wa wanafunzi hao (jina tunalo) alisema walielezwa na walimu wao kwamba ye yote ambaye hatokuwa amelipa ada na michango mbalimbali shuleni hapo ikiwemo mchango wa mlinzi hatoruhusiwa kufanya mitihani hiyo mpaka pale wazazi wao watakapokuwa wamelipa michango wanayodaiwa.

Mwanafunzi huyo alifafanua kuwa hata pale walipojaribu kuwaomba walimu wawaruhusu kufanya mitihani kwa vile suala la michango si jukumu lao bali la wazazi waligoma huku wakibeza agizo la serikali lililotolewa hivi karibuni la ‘matokeo makubwa sasa’ (Big result now).

“Tuliwabembeleza sana walimu waturuhusu kufanya mitihani hasa wale wa kidato cha nne na cha pili kwamba matokeo ya mitihani hiyo kwa kawaida hujumuishwa na matokeo ya mwisho ya kumaliza kidato cha nne na wale wa cha pili, waligoma,”

“Binafsi niliwaeleza kuwa hivi sasa serikali imetangaza mpango wa matokeo makubwa sasa, lakini walimu hao walibeza na kueleza bila michango kulipwa hakuna Big results now, tulishangaa, tukaambiwa wote ambao hatujalipa michango na ada tukae chini uwanjani, hawakujali jua, kisha tukapewa kazi ya kumwagilizia bustani,” alieleza mwanafunzi huyo.

Kwa upande wake mkuu wa shule msaidizi Kasuka Masanja alikiri kuzuiwa kwa watoto hao kufanya mitihani kutokana na wazazi wao kutokulipa michango waliyotakiwa kulipa lakini hata hivyo alidai mitihani hiyo siyo halisi bali ilikuwa ni majaribio ili kuwashinikiza wazazi kulipa ada na michango wanayodaiwa.

Akizungumzia hali hiyo ofisa elimu sekondari manispaa ya Shinyanga Victor Emmanuel alishangazwa na taarifa za watoto hao kuzuiwa kufanya mitihani yao na kwamba ni kinyume na maelekezo yaliyotolewa na serikali.

“Siamini kama kweli wanafunzi hao wamezuiwa kufanya mitihani yao, si utaratibu, suala la michango haliwahusu watoto, ni la wazazi na tuliishatoa maelekezo ya jinsi ya kufuatilia michango hiyo kwa wazazi kwa utaratibu wa kuwasiliana na viongozi wa serikali katika kata, hairuhusiwi kabisa watoto kurudishwa nyumbani kwa kutolipa ada ama michango,” alieleza Emmanuel.

Hata hivyo Emmanuel aliahidi kulifuatilia tatizo hilo ili kuweza kubaini ukweli wake ambapo alitoa wito kwa shule nyingine kutozuia wanafunzi kufanya mitihani yao kwa sababu ya wazazi wao kushindwa kulipa ada ama michango au kuwapa adhabu ya aina yoyote kwa makosa ambayo siyo ya kwao
Endelea Kusoma >>

UZINDUZI WA RIPOTI YA MAENDELEO YA BINADAMU TANZANIA THDR

0 comments
NAIBU SPIKA  WA BUNGE JOB NDUGAI AKIFUNGA SEMINA YA  UZINDUZI WA MCHAKATOWA RIPOTI YA MAENDELEA YA BINADAMU TANZANIA  THDR UZINDUZI HUO ULIANDALIWA NA TAASISI YA UTAFITI YA MASAUALA YA KIUCHUMI NA KIJAMII ESRF ULIFANYIKA KWENYE MJINI DODOMA LEO KUTOKA KULIA  MKURUGENZI WA UNDP TANZANIA PHLIPPE POINST WA PILI KULIA NI WAZIRI WA FEDHA DR WILLIAM MGIMWA,WSA KWANZA KUSHOTO NI MKURUGENZI MTENDAJI WA TAASISI YA UTAFITI WA MASUALA YA KIUCHUMI NA KIJAMII ESRF DR HOSEANA LUNOGELA NA WAZIRI WA ULINZI  SHAMSI VUAI


BAADHI YA WAJUMBE WA TAASISI YA UTAFITI YA MASUALA YAKIUCHUMI NA KIJAMII YA ESRF WALIOHUDHURIA UZINDUZI WA MCHAKATO WA RIPOTI YA MAENDELEO YA BINADAMU TAMZAMIA THDR ULIOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA PIUS MSEKWA MJINI DODOMA LEO

PICHA YA PAMOJA YA WABUNGE PAMOJA NA VIONGOZI WA TAASISI YA UTAFITI YA MASUALA YA KIUCHUMI NA KIJAAM  MARA BAADA YA UZINDUZI WA MCHAKATOWA RIPOTI YA MAENDELEO YA BINADAMU TANZANIA ILIYOFANYIKA MJINI DODOMA


 WZ

WAZIRI WA ULINZI  SHAMSI NAHODHA VUAI AKIZINDUA MCHAKATO WA RIPOTI YA MAENDELEO YA BINADAMU TANZANIA  ULIANDALIWA NA TAASISI YA UTAFITI YA MASUALA YA KIUCHUMI NA KIJAMII ESRF ULIOFANYIKA MJINI DODOMA

BAADHI YA WAJUMBE WA TAASISI YA UTAFITI YA MASUALA YAKIUCHUMI NA KIJAMII YA ESRF WALIOHUDHURIA UZINDUZI WA MCHAKATO WA RIPOTI YA MAENDELEO YA BINADAMU TAMZAMIA THDR ULIOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA PIUS MSEKWA MJINI DODOMA LEO KUSHOTO NI KATIBU MKUU WA WIZRAYA FEDHA DKT SERVACIUS LIKWELILE

BAADHI YA WAJUMBE WA TAASISI YA UTAFITI YA MASUALA YAKIUCHUMI NA KIJAMII YA ESRF WALIOHUDHURIA UZINDUZI WA MCHAKATO WA RIPOTI YA MAENDELEO YA BINADAMU TAMZAMIA THDR ULIOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA PIUS MSEKWA MJINI DODOMA LEO

Endelea Kusoma >>
0 comments

MTWARA WAIPOKEA KWA SHANGWE SEMINA YA FURSA KWA VIJANA


Meneja Kiongozi,Uhusiano NSSF Makao makuu jijini Dar, Eunice Chiume  akizungumza mapema leo kwenye semin ya FURSA iliyofanyika kwenye ukumbi wa Pentecoste Ligula B,uliopo mkabala na Kituo cha Vijana Mtwara,kulia ni Meneja wa NSSF mkoani Mtwara Bwa.Stanley Mullanzi na kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Vipindi Clouds Media Group,Ruge Mutahaba pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iramba (ambaye pia ni mzaliwa wa Newala mkaoni Mtwara),Mh.Yahya Nawanda wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikijadiliwa ukumbini humo.Semina hiyo inaratibiwa na Clouds Media Group na kufadhiriwa na NSSF,Lake Oil,Zantel,MaxMalipo na wengineo imewashirikisha wadau mbalimbali wa Mtwara na vitongoji vyake wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya.
  Baadhi ya Wakazi wa Mji wa Mtwara na vitongoji vyake wakifuatilia kwa makini  yaliyokuwa yakijiri kwenye semina ya Fursa kwa Vijana iliyofanyika mapema leo ndani ya ukumbi wa  Pentecoste Ligula B,uliopo mkabala na Kituo cha Vijana mkoani Mtwara.
 Mkuu wa Wilaya ya Iramba (ambaye pia ni mzaliwa wa Newala mkaoni Mtwara),Mh.Yahya Nawanda akizungumza na wakazi wa mji wa Mtwara waliojitokeza kwa wingi kwenye semina ya Fursa kwa Vijana mapema leo,Mh.Yahya alizunguma mengi zikiwemo fursa mbalimbali zinazopatikana ndani ya mkoa wa Mtwara na Singida namna ya kuzifanyia kazi katika suala zima la kujikwamua na maisha. 
Mkurugenzi wa Vipindi Clouds Media Group,Ruge Mutahaba  akihitimisha semina ya Fursa kwa Vijana mapema leo mchana,ndani ya ukumbi wa ukumbi wa Pentecoste Ligula B,uliopo mkabala na Kituo cha Vijana Mtwara,kulia kwake ni Meneja Kiongozi,Uhusiano NSSF Makao makuu jijini Dar,Eunice Chiume pamoja na Meneja wa NSSF mkoani Mtwara Bwa.Stanley Mullanzi.Semina ya Fursa kwa vijana tayari imekwishafanyika mikoa ya Tabora,Kigoma,Singida na sasa Mtwara.
PICHA ZAIDI BOFYA MICHUZIJR.BLOGSPO.COM

WAJUMBE WA BARA WAENDA ZANZIBAR KWENYE BARAZA KUU LA UMOJA WA VIJANA WA CCM, TAIFA

 Baadhi ya wajumbe wakiwa Makao Makuu ya UVCCM, jijini Dar es Salaam, tayari kwa safari ya kwenda Zanzibar kwenye kikao cha Baraza Kuu ya Jumuia hiyo, kitakachofanyika kesho.
 Wajumbe wakiwa nje za jengo la Umoja wa Vijana wa CCM, mjini Dar es Salaam, kabla ya kuanza safari yao kwenda Zanzibar
 Baadhi ya wajumbe wakiwa Ofisi za UVCCM mjiniu Dar es Salaam, kabla ya kuondoka kwenda Zanzibar kwenye kikao hicho.
 Wajumbe wakiwa kwenye ofisi ya UVCCM makao makuu
Baadhi ya wajumbe wakipanda mabasi kutoka makao makuu ya UVCCM kwenda Bandarini kubanda boti kwenda Zanzibar kwenye kikao hicho cha Baraza Kuu la UVCCM leo
Baadhi ya wajumbe wakiwa bandari ya Dar es Salaam, kupanda boti
Wajumbe wakiwa kwenye boti mjini Dar es Salaam, tayari kwa safari ya Zanzibar
Wajumbe wakiwa kwenye boti yatari kwa safari ya Zanzibar. Imetayarishwa na theNkoromo Blog
Endelea Kusoma >>
0 comments

RAIS JAKAYA KIKWETE APOKEWA NA GWARIDE LA SUNGUSUNGU WA AUSTRIA

 Taswira za askari wa jadi wa jimbo la Tyrol huko Alpbach nchini Austia wakiingia kwa gwaride rasmi lililoandaliwa kwa heshima ya Rais Jakaya Kikwete aliye katika mkutano wa Kamisheni ya Ulaya mjini humo. Historia ya askari hawa, wanaojulikana kama Schuetzenkompanie, inakwenda miaka ya 1810 wakati wa vita na watu wa Bavaria. Soma historia yao BOFYA HAPA
 Sungusungu hao wakiendelea kuwasili
 Kila mmoja ana gobole lililotengenezwa kienyeji
 Watoto kwa wakubwa wamevutiwa na Sungusungu hao
 Gwaride rasmi
 Mdau anajiunga na Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Austria Mhe Heinz Fischer (katikati), Rais wa Kamisheni ya Ulaya Mhe Jose Manuel Barroso (wa pili kushoto), Rais wa Mkutano wa Alpbach Dr Franz Fischer (kushoto) pamoja na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akifuatiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala
Endelea Kusoma >>
0 comments

LIGI DARAJA LA KWANZA CHANETA CUP KUHITIMISHWA KESHO UWANJA WA SOKOINE, MULUGO KUWA MGENI RASMI.

Mwenyekiti wa Chama cha Netboli Taifa(CHANETA) Annah Kibira anawaomba wapenzi wa mpira huo Mkoa wa Mbeya kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Sokoine kwa sherehe za kufunga ligi hiyo.
Mwenyekiti wa Chaneta Mkoa wa Mbeya, Mary Mng’ong’o amesema Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo Philipo Mulugo ambaye atashuhudia michezo miwili na kugawa zawadi kwa washindi.
Viongozi wa chaneta wakiongea na waandishi wa habari

Mwenyekiti wa Chama cha Netboli Taifa(CHANETA) Annah Kibira anawaomba wapenzi wa mpira huo Mkoa wa Mbeya kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Sokoine kwa sherehe za kufunga ligi hiyo.
Kibira amesema ligi hiyo itahitimishwa kwa michezi miwili ambayo ni kati ya Hamambe dhidi ya Jeshi Staa na mchezo mwingine kati ya Filbert Bayi dhidi ya JKT Mweni.
Amesema katika michezo hiyo mgeni rasmi ambaye anatarajiwa kuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo atashuhudia michezo hiyo kwa kuzikakugua timu hizo kabla ya kutoa zawadi kwa washindi na kufunga.
Hata hivyo Kibira ametoa wito kwa wadau wa michezo nchini kujitokeza kudhamini ligi hiyo ili kuwa na mvuto kama michezo mingine ili kuzifanya timu shiriki kuwa nyingi.
Kibira amesema kukosekana kwa wafadhili wa Ligi za Netboli kumechangia timu kupungua katika Ligi daraja la Kwanza mwaka huu ambapo kwa kawaida zilitakiwa kuwa na timu 20 lakini hadi ligi inafunguliwa Agosti 24, Mwaka huu jumla ya timu 12 zilijitokeza na kushiriki ligi hiyo itakayohitimishwa Septemba Mosi, Mwaka huu.
Alisema kutokana na kushiriki kwa timu chache jumla ya michezo 66 ikakuwa imefanyika kufikia kesho kwa amani, Upendo na Mshikamano ukihusisha timu 12 na kuongeza kuwa kwa mujibu wa Kanuni za Chaneta timu nane ambazo zilishindwa kushiriki zinatakiwa kushuka daraja hivyo hatima yao Kamati tendaji itaamua.
Akizungumzia kilele cha kuhitimisha Ligi hiyo Mwenyekiti wa Chaneta Mkoa wa Mbeya, Mary Mng’ong’o amesema Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo Philipo Mulugo ambaye atashuhudia michezo miwili na kugawa zawadi kwa washindi.
Mng’ong’o amesema undeshaji wa ligi hiyo umekutana na changamoto nyingi lakini kubwa kabisa ni ukosefu wa fedha uliotokana na uchangiaji duni wa wadau hali iliyopelekea timu kujigharamia zenyewe.
Aidha ametaja msimamo wa ligi hiyo kuwa inaongozwa na timu ya JKT Mbweni yenye alama 20 sambamba na timu ya Filbert Bayi yenye alama 20 lakini ikiwa na magoli machache dhidi ya JKT Mbweni.
Timu ya Magereza Morogoro inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 17 ikifuatiwa na Jeshi Staa yenye alama 15 na timu mwenyeji ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya (HAMAMBE) ikishika nafasi ya tano kwa alama 13 huku timu ya Polisi Mbeya ikifunga mkia kwa alama 2 sambamba na CMTU kutoka Dar Es Salaam ikiwa haina alama hata moja.

Na Mbeya yetu

Endelea Kusoma >>

Friday, August 30, 2013

0 comments

Waasi wa M23 kusitisha mapigano DRC


 
Wapiganaji wa M23
Waasi wa M23 Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamesema kuwa watasitisha mapigano, kufuatia makabiliano makali na wanajeshi wa serikali wanaoungwa mkono na wanajeshi wa Umoja wa Mataifa.
Afisa mmoja wa Kundi hilo la M23 Museveni Sendugo, ameiambia BBC kuwa wanajeshi wake tayari wamerudi nyuma umbali wa kilomita tano kutoka eneo la mapigano.
Kiongozi wa kundi hilo Bertrand Bisima amesema uamuzi huo utaruhusu wachunguzi huru kupeleleza jinsi makombora yalivyorushwa nchini Rwanda siku ya Alhamisi.
Serikali ya Rwanda imesema jeshi la Congo lilirusha makombora hayo, madai ambayo yamekanusha na serikali ya Congo.
Wengi wa wapiganaji wa M23 ni wanajeshi walioasi jeshi la serikali, wengi wao wakiwa wa kibila la Kitutsi sawa na uongozi wa Rwanda.
Serikali ya DRC na Umoja wa Mataifa zimeishutumu serikali ya Rwanda kwa kuwaunga mkono wapiganaji wa kundi hilo la M23, tuhuma ambazo zimekanushwa na utawala wa Kigali
.
Wanajshi wa Umoja wa Mataifa nchini DRC
Awali, katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametoa wito kwa rais wa Rwanda, kuwa mvumilivu huku uhasama kati yake na nchi jirani ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ukiendelea kutokota katika maeneo ya mipakani.
Bwana Ban, alizungumza na rais Paul Kagame baada ya serikali yake kuishutumu Congo, kwa kufanya shambulio katika ardhi yake makusudi na kumuua mama mmoja na kumjeruhi mtoto wake.
Msaidizi wa katibu huyo mkuu wa Umoja wa Mataifa, amenukuliwa akiiambia Umoja wa Mataifa kuwa wapiganaji wa kundi la waasi wa M23, wameonekana wakirusha makombora wakilenga Rwanda.
Serikali ya DRC na Umoja wa Mataifa zimeshutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi hao wa M23, madai ambayo yamepingwa vikali ya utawala wa Kigali.
Wanajeshi wa Congo wakishirikiana na wanajeshi wa Umoja wa Mataifa, wamekuwa wakifanya mashambulio dhidi ya waasi hao wa M23 karibu na mpaka wa Rwanda, tangu wiki iliyopita.

Waasi walengwa na UN

Kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kutunza amani nchini DRC, Monusco, kiliimarishwa zaidi pale wanajeshi elfu tatu zaidi walipotumwa nchini humo kupambana na waasi hao.
Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda Louise Mushikiwabo, amesema mabomu na makombora kumi na tatu yalirushwa katika ardhi yake siku ya Jumatano na mengine kumi siku ya Alhamisi.

Rais wa Rwanda Paul Kagame akiwa na Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa
Waziri huyo amedai kuwa kufikia sasa wanajeshi hao wa Congo wamefanya mashambulio thelathini na nne nchini Rwanda.
Amewashutumu wanajeshi wa DRC kwa kuwalenga raia wake na kusisitiza kuwa kwa sasa wanajiepusha kulipisa kisasi lakini hawatasita kujibu ikiwa uchokozi huo hautakoma.
Msemaji wa jeshi la Congo Kanali Olivier Hamuli ameiambia BBC kuwa jeshi lake haliwezi kurusha makombora kulenga maeneo yanayokaliwa na raia.
''Waasi ndio wanaoweza kufanya kitendo kama hicho, wapiganaji wa M23 na wala sio wanajeshi wake ndio waliokuwa katika eneo ambalo makombora hayo yalirushwa'' Alisema Kanali Hamuli.
Matamshi hayo yaliungwa mkono na msaidizi wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Mulet ambaye aliiambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa, wanajeshi wake nchini DRC walishuhudia wapiganaji wa M23, wakirusha makombora wakilenga Rwanda na wala sio wanajeshi wa Congo.
Takriban watu laki nane wamekimbia makwaoi nchini Congo tangu waasi hao wa M23 kuanzisha mashambulio katika eneo la Mashariki mwa Congo Aprili mwaka wa 20120.
You might also li
Endelea Kusoma >>
0 comments

.

ETO'O ATAMBULISHWA RASMI CHELSEA NA KUKABIDHIWA UZI WA BLUU

IMEWEKWA AGOSTI 30, 2013 SAA 10: 57 JIONI
MSHAMBULIAJI Samuel Eto'o amesainisi Mkataba wa mwaka mmoja na Chelsea jana kwa mshahara wa Pauni Milioni 7 kwa mwaka.
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 32 ametambulishwa rasmi leo baada ya kukamilisha vipimo vya afya.
Mwanasoka huyo bora mara nne Afrika ambaye aliwasili London juzi usiku kwa treni kutoka Ufaransa hadi Stesheni ya St. Pancras, alisema: "Nimeona ubora ambao wanao Chelsea, na nimekuwa nikimfurahia sana Jose Mourinho kabla, hivyo wakati nafasi inapotokea, huwa nafurahia kuichukua.
Parading: Eto'o has signed for Chelsea
Uzi wa bluu: Eto'o akiwa na jezi ya Chelsea
Pen to paper: Eto'o signs the contract in the presence of Chelsea club secretary and director David Barnard
Anamwaa wino: Eto'o akisaini Mkataba na Katibu wa Chelsea, David Barnard
Pleased to be here: Eto'o has signed on a free transfer
Raha kuwa hapa: Eto'o amesaini kama mchezaji huru
Endelea Kusoma >>

WABUNGE WALIOKUWA MSTARI WA MBELE KUTAKA MSWADA UREKEBISWHE LEO

0 comments
 WABUNGE WALIOKUA MSTARI WA MBELE KUPINGA NA KUTAKA MABADILIKO YA MSWADA WA SERIKALI WA SHERIA YA UMWAGILIAJI ULIOWAKILISHWA NA KUSOMWA NA WAZIRI WA KILIMO NA UMWAGILIAJI NA MSWADA HUO KUPITA KWA TAABU  AMBAO ULIONGEZWA MUDA KATIKA DAKIKA ZA MAJERUHI BAADA KUPATIKANA KWA MUAFAKA LEO BUNBGENI MJINI DODOMA
MBUNGE WA JIMBO LA KISARAWEMBUNGE ALIETAKA  MUSWADA HUOUREKIBISHWE

WAZIRI WA KILIMO NA UMWAGILIAJI CHRISTOPHER CHIZA ALIBANWA NA WABUNGE KUHUSU MSWADA WA SHERIA YA UMWAGILIAJI

WABUNGE WA KAMBI YA UPINZANI


MBUNGE WA JIMBO LA SIMANJIRO OLE SENDEKA

MBUNGE JIMBO LA PERAMIHO JENISTER MUHAGAMA

MBUNGE WA JIMBO LA KAWE HALIMA MDEE

MBUNGE WA JIMBO LA KISESA LUHOGA MPINA

 
MBUNBGE WA JIMBO LA NGASI ALI KESSIKASKAZINI

Endelea Kusoma >>

MABARAZA YA KATIBA

0 comments


Baadhi ya akina mama wamakundi ya wajane na watoto walio katika mazingira hatarishi  wakimsikiliza naibu waziri wa sheria na katiba Angela kairuki wakati wa uchangiaji wa rasim ya katiba  ya jamhuri ya Tanzania wakati wa mabaraza ya katiba ya kata
  Naibu waziri wa sheria na katiba Angela Kairuki akifungua mkutano wa akina mama wajane na watua walioathirika na maradhi mkoani dodoma mkutano huo ulifanyika kanisa la rutharani  Arusha ya ukimwi mkutano  huo uliafinywa kwa kupitia rasimu ya katiba ya jamhuri mpya na kutoa mapendekezo yao

 baadhi ya akina mama wakipiga kupiga makofi na kufurahia kupekewa rasim



 naibu waziri wa sheria na katiba akiagana na wansema wa hapa mkoani dodoma

Endelea Kusoma >>
0 comments

CCM; TUTAWASAIDIA WAZEE

 Baadhi ya wawakilishi wa Mtandao wa Wazee wakiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye nje ya ofisi za Makao Makuu ya Chama Dodoma leo tarehe 30 Agosti 2013.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na mmoja wa wawakilishi wa Mtandao wa Wazee Bibi Koku , Wazee hao walifika Makao Makuu ya CCM kuja kuzungumza madai ya mafao yao ambayo waliahidiwa na serikal
Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu