Wednesday, October 30, 2013

Majaji kutoa uamuzi wa hukumu ya kesi ya Babu Seya na mwanae itakavyopangwa

0 comments
Askari wa magereza wakimueka katika ilinzi mkali papii kocha mtoto wa vicking nguza wakati wakitolewa katika mahaka ya fufaa

Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na mwanawe Johnson  Nguza au Papii wakitolewa  katika chumba cha Mahakama ya Rufaa Tanzania jijini Dar es Salaam leo, baada ya  kusikilizwa kwa rufaa yao ya kuitaka mahakama hiyo kupitia upya hukumu iliyotolewa Februari 10-2010 na mahakama hiyo. Nguza na Papii walihukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya ubakaji na ulawiti. 

Babu seya  nguza vicking akiwa na mwanae Johnson Nguzo wakitoka kwenye mahakama ya rufaawakirudishwa tena gerezani kusubiri kesi yao itakapo somwa tena










awakingia katika mahakama kuu kusubiri kurudishwa gerezani

picha zote na mzuka wa fungo blog

Endelea Kusoma >>
0 comments
RAIS WA CAF AMPONGEZA MALINZI

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Issa Hayatou amempongeza Jamal Malinzi kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 27 mwaka huu.



Katika salamu zake kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya CAF na familia ya mpira wa miguu Afrika, Rais Hayatou amesema uchaguzi huo unampa Rais Malinzi fursa ya kuupeleka mbele mpira wa miguu nchini Tanzania.



Amesema CAF ina imani uwezo wake katika uongozi, uzoefu na ujuzi katika mpira wa miguu havitausaidia mpira wa miguu Tanzania pekee bali Afrika kwa ujumla, na kuongeza kuwa ataendeleza ushirikiano uliopo ili kuwanufaisha zaidi vijana wa bara hili.



Rais Hayatou amemtakia Rais Malinzi kila la kheri katika kipindi chake cha uongozi na kumhakikishia kuwa CAF iko pamoja naye katika kusukuma mbele gurudumu la kuendeleza mpira wa miguu.



PAMBANO LA YANGA, MGAMBO SHOOTING LAINGIZA MIL 37/-

Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Mgambo Shooting lililochezwa jana (Oktoba 29 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 37,915,000.



Washabiki waliohudhuria mechi hiyo namba 46 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 walikuwa 6,515 ambapo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.



Mgawo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 5,783,644.07, gharama za kuchapa tiketi sh. 3,145,790 wakati kila klabu ilipata sh. 8,550,741.95.



Wamiliki wa uwanja walipata sh. 4,347,834.89, gharama za mchezo sh. 2,608,700.93, Bodi ya Ligi sh. 2,608,700.93, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,304,350.47, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,014,494.81.



SIMBA, KAGERA SUGAR KUUMANA KESHO

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaanza raundi ya 12 kesho (Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Simba na Kagera Sugar itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.



Viingilio katika mechi hiyo itakayooneshwa moja kwa moja na Azam Tv kupitia TBC 1 vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A.



Nayo Yanga itashuka uwanjani Novemba Mosi mwaka huu katika mechi nyingine ya ligi hiyo dhidi ya JKT Ruvu itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



Novemba 2 mwaka huu kutakuwa na mechi nne; Mgambo Shooting na Coastal Union (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Tanzania Prisons na Oljoro JKT (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).



Raundi hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Mbeya City itakuwa mwenyeji wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.



Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7 mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashani United vs Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, Rhino Rangers vs Tanzania Prisons na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.



Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City wakati Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



Boniface Wambura Mgoyo

Ofisa Habari

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

 

Endelea Kusoma >>

Monday, October 28, 2013

AZAM YAIBAMIZA SIMBA BAO 2-1 LEO

0 comments
KAMA SENEMA SIMBA AKIFUNGWA BAO LA PILI NA AZAM HUKU WAKIDUWAA KIPA BILA KUJUA ULIMPITAJE WAKATI WA NCHEZO WA LIGI KUU YA VODACOM ULIOCHEZWA LEO KWEWNYE UWANJA WA TAIFAAZAM 2-1

MCHEZAJI WA ZAHORO PAZI WA SIMBA KUSHOTO WAKIKABANA NA NA MCHEZAJI WA AZAM AGRRY MORIS WAKATI WA PAMBANOLA LIGI KUU YA VODACOM ILIYOCHEZWAKWENYE UWANJA WA TAIFA LEO TIMU YA AZAM IMETUNGUA KWA BAO 2-1

Endelea Kusoma >>
0 comments

 
MSAFARA WA WAZIRI NCHIMBI HAUKUPIGWA MAWE SONGEA
Habari iliyotolewa Oktoba 26, mwaka huu na baadhi ya magazeti na mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari ‘Msafara wa Waziri Nchimbi wapigwa mawe Songea’ si za kweli bali zimetengenezwa na walizituma kwa nia ya kupotosha jamii.
Oktoba 25, mwaka huu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Dk. Emmanuel Nchimbi alitembelea Miradi ya Maendeleo pamoja na kufanya Mkutano aliianza katika Kata ya Mletele na kumalizia Kata ya Matarawe, katika jimbo lake la Songea Mjini. Wakati alipomaliza mkutano wake wa Mletele alitaarifiwa makundi ya watu yamefunga njia katika daraja la Matarawe na wamesema hawatalifungua mpaka Mhe Nchimbi akaliangalie na kuzungumza nao.
Mhe. Nchimbi alishauriwa kubadili njia ili kuwahi mkutano wa hadhara wa Matarawe ambapo wananchi walikuwa wanamsubiri kwa zaidi ya saa mbili. Pamoja na kushauriwa kupita njia nyingine, Mhe. Nchimbi aliamua kwenda kuwasikiliza, alifika katika eneo la daraja akiwa amefuatana na viongozi mbalimbali wa Manispaa na Serikali, mhe Nchimbi aliwapa fursa wananchi hao kueleza kero zao, nao walimwambia kuwa eneo hilo limekuwa na ajali mara kwa mara tokea barabara ya lami ilipokamilika na kusababisha vifio vya watu karibu wanne hivyo walimuomba mbunge wao awasaidie kumaliza kero hiyo.  
Akijibu kero hiyo, Mhe. Nchimbi aliwaambia wananchi wake kuwa ni yeye aliyefanikisha ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami atalishughukia tatizo hilo pia na kuwa amelichukua kwa uzito mkubwa. Baada ya majibu ya mhe Nchimbi wananchi hao waliridhika na ndipo wenyewe wakafungua barabara na kutoa vizuizi ili waziri na msafara wake waweze kupita. Mhe Nchimbi na ujumbe wake waliendelea na safari na kwenda kwenye mkutano wa hadahara takribani mita 200 toka daraja hilo. Saa moja baada ya mhe Nchimbi kuwa ameshapita baadhi ya vijana walifunga tena barabara na ndipo Jeshi la Polisi lilipolazimika kuwatawanya na kuwakama vijana saba.
Waandishi wa habari wa Televisheni za Star TV, Channel Ten na TBC wanamikanda ya tukio zima na hivyo mikanda hiyo inaweza kuthibitisha habari kuwa mhe Nchimbi alipigwa mawe ni uzushi mtupu.
Waziri Nchimbi alikuwa katika ziara ya kawaida jimboni kwake na aliweza kufanya mikutano minane ya hadhara iliyohudhuriwa na mamia ya watu na iliendeshwa kwa utulivu mkubwa ambapo wenyeviti wa mikutano hiyo walikuwa madiwani wa kata husika, ambapo katika kata sita mikutano hiyo iliongozwa na madiwani wa CCM na kata mbili iliongozwa na madiwani wa Chadema.
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inavisihi vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kujiridhisha na ukweli wa taarifa wanazozipata kabla ya kuzitoa kwa wananchi ili wananchi waweze kupata haki yao ya kupata habari zilizokuwa sahihi.
 Mwisho.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
28 Oktoba, 2013
Endelea Kusoma >>

Sunday, October 27, 2013

MATEMBEZI YA HISANI YA SARATANI YALIYOFANYIKA LEO DAR

0 comments















Endelea Kusoma >>

MAHAFALI YA WAMA NAKAYAMA NYAMISATI

0 comments
WATU MBALIMBALI WAKICHEZA NA NYOKA  WAKATI WA SHEREHE YA MAHAFALI YA WAMA NAKAYAMA n

WAGENI WALIOFIKA KWENYE MAHAFALI

WANAFUNZI WAKIWA NA VYETI VYAO

Endelea Kusoma >>

MAHAFALI YA SHULE YA WAMA NAKAYAMA YALIVYOFANA

0 comments
MBUNGE WA VITI MAALUM VICK KAMATA PAMOJA NA MWENYEKITI WA WAMA MAMA SALMA KIKWETE

IGIZO LA MCHEZO WA MWANAFUNZI ALIEKAATA KUDANGANYWA NA MAFATAKI


wanafunzi wakicheza na mwenyekiti wa WAMA MAMA SALMA KIKWETE WAKATI WA MAHAFALI YA KWANZA YALIYOFANYIKA NYAMISATI

BAADHI YA WAGENI WALIOFIKA KWENYE MAHAFALI YA SHULE HIYO

RAIS DR JAKAYA KIKWETE AKIOIWAELEZA WAGENI WAKAE MKAO WA KUPIGWA PICHA PAMOJA


baadhi ya wageni kutoka kijiji cha nyamisati

Endelea Kusoma >>

Friday, October 25, 2013

0 comments
Sehemu ya mamia ya wananchi wa Kata ya Mjini, Manispaa ya Songea wakiwa tayari kwa kumsikiliza Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini (CCM) ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi. Dk Nchimbi baada ya kuzindua barabara yenye kiwango cha lami yenye urefu wa mita 600 ambayo imegharimu zaidi ya Sh75 milioni, pia mbunge huyo ameweka jiwe la msingi katika ofisi ya Kata ya Mateka. Dk Nchimbi katika ziara yake ya siku tano jimboni humo, pia anatarajiwa kuzindua ujenzi wa mabweni ya sekondari pamoja na nyumba za walimu.
 

Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini (CCM) ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akikata utepe kuashiria uzinduzi wa barabara ya lami ambayo inamaliziwa kujengwa yenye urefu wa mita 600 iliyopo katika Kata ya Mjini, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma. Barabara hiyo imegharimu zaidi ya Sh75 milioni. Dk Nchimbi yupo mjini Songea kwa ziara ya siku tano akikagua pamoja na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo jimboni mwake.
 

                                                                 
Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini (CCM) ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (aliyevaa miwani) akiwa na Diwani wa Kata ya Mjini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Ruvuma, Joseph Fuime (kulia kwa Dk Nchimbi) wakipita kwa furaha barabara aliyoizindua Dk Nchimbi mjini Songea mkoani mjini Songea leo. Barabara hiyo yenye kiwango cha lami ina urefu wa mita 600 ambayo imegharimu zaidi ya Sh75 milioni, pia mbunge huyo ameweka jiwe la msingi katika ofisi ya Kata ya Mateka. Dk Nchimbi pia anatarajiwa kuzindua ujenzi wa mabweni ya sekondari pamoja na nyumba za walimu

Endelea Kusoma >>
0 comments
MWENYEKITI WA CCM TAIFA RAIS JAKAYA KIKWETE AFUNGA MAFUNZO KWA WATENDAJI NA VIONGOZI WA CCM DODOMA

Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete wakati akifunga  mafunzo kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, usiku wa kuamkia leo Oktoba 25, 2013 katika ukumbi wa mikutano wa CCM wa ‘White House’ mjini Dodoma. Mafunzo hayo yaliyokuwa ya siku nne yalifunguliwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein. Kulia kwake  ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Philip Mangula na kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana. PICHA NA IKULU
Endelea Kusoma >>
0 comments


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS


 
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Kikwete: Kero hii imetosha, sasa ni kitabu kimoja mwanafunzi mmoja
·        Asema tunao wanasiasa wa kutosha, sasa tunahitaji wanasayansi

·        Aaagiza viongozi katika ngazi zote kutenga fedha za kuwajengea walimu nyumba katika bajeti zao

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Serikali yake itakomesha kero ya wanafunzi na watoto wa shule nchini kuchangia vitabu vya kiada katika masomo yao.

Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa wajibu wa kuhimiza ujenzi wa maabara za sayansi katika shule nchini siyo tu matakwa ya Rais bali suala hili linatakiwa kuwa wajibu wa kufa na kupona kwa kila kiongozi katika ngazi zote za uongozi kwa sababu nchi haiwezi kuendelea bila wanasayansi.

Vile vile, Rais Kikwete amewaagiza viongozi wote katika ngazi zote na hasa kwenye ngazi ya wilaya na halmashauri kutenga katika bajeti zao fedha za kujenga nyumba za walimu kwa nia ya kuboresha mazingira ya kazi ya walimu nchini.

Rais Kikwete amesema na kutoa maagizo hayo jana, Jumatano, Oktoba 23, 2013, alipozungumza na uongozi wa Mkoa wa Njombe wakati anakamilisha na kujumuisha ziara yake ya siku saba katika Mkoa huo kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe.

Rais ambaye alizungumza masuala mengi kuhusiana na aliyoyaona wakati wa ziara hiyo alijielekeza kwa muda mrefu katika masuala ya elimu na nafasi ya viongozi katika kusuma mbele sekta ya elimu kama mkombozi mkuu wa Watanzania.

Kuhusu kupatikana kwa vitabu vya kiada kwa watoto na wanafunzi nchini, Rais Kikwete amewaambia viongozi hao wa Njombe:

“Nimeilekeza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi kuwasilisha kwangu bajeti inayotakiwa kutuwezesha sisi, kama Taifa, kuhakikisha kuwa kila mtoto wetu na mwanafunzi wa nchi yetu hii anakuwa na kila kitabu cha kiada kwa kila somo.”

“Hili ni jambo ambalo tumelizungumza kwa muda mrefu. Hakuwezi kamwe kuendelea kuahirisha majawabu ya suala hili. Nataka kujua itatugharimu kiasi gani kwa kila mtoto na mwanafunzi nchini kuwa na kitabu chake cha kiada kwa kila somo. Tumepata msaada wa marafiki wetu. Tunawashukuru. Lakini sasa wakati umefika kwa sisi wenyewe kuelekeza nguvu zetu zote kumaliza tatizo hilo,” amesema Rais Kikwete na kusisitiza:

“Ilikuwa wanafunzi 10 kwa kitabu kimoja, tumeshuka hadi wanafunzi watatu kwa kitabu kimoja. Hili halitoshi na hali hii haikubaliwi ni lazima iwe ni mwanafunzi mmoja na kitabu kimoja, kitabu chake.”

Kuhusu ujenzi wa maabara ya sayansi katika kila sekondari nchini na umuhimu wa kufundisha masomo ya sayansi nchini, Rais Kikwete amesema “ni lazima tujenge hizi maabara haraka, ni lazima tuongeze kasi yetu ya kufundisha masomo ya sayansi na ni lazima tukabiliane na uhaba wa walimu wa kufundisha sayansi nchini.”

“Maendeleo ya nchi huletwa na wanasayansi. Na kama mfumo wa elimu wa nchi yoyote hautoi nafasi ya kutosha kulea na kujenga wanasayansi basi nchi hiyo inapiga hatua ya kurudi nyuma. Kwenye hili, tayari tumeachwa na treni na wala suala hili siyo matakwa ya Rais bali ni suala la kufa na kupona kwa viongozi wote wa ngazi zote,” amesema Rais Kikwete.

Ameongeza: “Siyo kila mtu katika nchi yetu atakuwa mwanasiasa. Hawa tayari tunao wa kutosha na wengine kazi yao sasa ni kusababisha ghasia nchini. Tunahitaji wanasayansi zaidi – tunahitaji madaktari, tunahitaji wahandisi. Ni lazima tuwekeze ipasavyo katika eneo hili kwa sababu tukikosea sasa tutakuwa tumekosa hatua moja kubwa na muhimu katika jitihada za kujiletea maendeleo.”

Amesema kuwa anatambua matatizo yaliyoko katika ufundishaji wa masomo ya sayansi nchini na kuwa kwa sababu hiyo ameitisha mkutano wa wadau wote wanaohusika na elimu na eneo la sayansi nchini ambao utafanyika Novemba 3, mwaka huu, kwa nia ya kutafuta majawabu ya matatizo hayo.

Tanzania inahitaji walimu 44,007 wa sayansi katika shule zake za sekondari. Waliopo kwa sasa ni walimu 17,059 na hivyo kuwepo na upungufu wa walimu 26,948 wakati vyuo vyote nchini vina uwezo wa kuhitimisha walimu 2,100 kwa masomo ya sayansi kila mwaka.

Kuhusu ujenzi wa nyumba za walimu, Rais Kikwete amesema kuwa kila kiongozi popote alipo ni lazima awe na mpango kabambe wa kuhimiza ujenzi wa nyumba za walimu na kuweka katika bajeti yake ya kila mwaka fedha za ujenzi huo.

“Kwenye ngazi ya taifa tumetoa Sh. Milioni 500 kwa kila Halmashauri nchini mwaka huu kama namna ya kuanza kukabiliana na tatizo hilo. Mwaka huu wa fedha, tunaanza kwa majaribio na Halmashauri 40 na ile ya Makete katika Mkoa huu wa Njombe ni mojawapo. Tutaendelea kutoka fedha kila mwaka huu kwa nia ya kumaliza tatizo hili.”

Ameongeza: “Sasa kwenye kila ngazi ya wilaya, kaeni chini mtafakari jinsi gani ya kuzitumia fedha hizo vizuri ili ziweze kujenga nyumba nyingi. Natambua kuwa kwenye sehemu nyingine shughuli hii itakuwa ngumu unapokuwa na madiwani ambao pia ni wakandarasi. Lakini hii tutakabiliana nalo.”

Ameelekeza kuwa mbali na kuzitumia fedha hizo vizuri, pia ametaka kila Halmashauri nchini kutenga fedha katika bajeti zao za ujenzi wa nyumba za walimu.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
Endelea Kusoma >>

Thursday, October 24, 2013

MTOTO ANAOMBA MSAADA WA KUTIBIWA HONOLINA MKAZI WA MGETA

0 comments



HUJAFA Hujaumbika! Mtoto Honolina Christian (11) yupo kwenye mateso makubwa na amewalilia Watanzania wote kuanzia Rais Jakaya Kikwete, serikali yake nzima na wanajamii akiwaomba msaada wa kumwezesha apate matibabu yatakayookoa maisha yake.
Mtoto huyo ambaye huwezi kumuangalia mara mbili bila kutokwa na machozi alisema tumaini lake ni kwa watu watakaoguswa na kilio chake akidai ameteseka vya kutosha na hivyo anadhani umefika muda na yeye afurahie maisha kama watoto wengine.
Akizungumza na MZUKA WA FUNGO akiwa ameongozana na mama yake, mtoto Honolina alisema maumivu anayopata kwa madonda yanayoitafuna ngozi yake yanamnyima raha na angeomba asaidiwe aweze kwenda kufanyiwa matibabu nje ya nchi ili na yeye apumue.
"Naumia...Nateseka na sijui niseme nini. Nawaomba Watanzania kuanzia Rais, Wabunge, Mawaziri na watu waliojaliwa uwezo wanisaidie niweze kupata matibabu, nimeteseka na ninateseka sana na ugonjwa huuu..." Honolata alisema huku akianza kulia kwa simanzi.
Mama yake mzazi aliyeambatana na mtoto huyo, Grace John alisema tangu mwanaye azaliwa Juni 12, 2002 hajawahi kufurahia maisha kutokana na maradhi yaliyomuandama katika namna ya ajabu kabisa.
"Kwanza alizaliwa akiwa amejaa nywele mwili mzima na baadaye nywele hizo kupukutika kisha mwili mzima kuwa kama ngozi ya chui na kumkimbiza hospitali ya Morogoro alipopewa mafuta ya ngozi kumtibia," alisema.
Mkazi huyo wa mkoani Morogoro, anasema tangu hapo mwanaye amekuwa akiteseka na kuharibika ngozi ikiwemo kuota pembe mbili kichwani na kuwa na ndimi saba zilizofanyiwa upasuaji KCMC kabla ya mapembe hayo kumuacha na mashimo kichwani yaliyolazimisha azibwe kwa ngozi ya pajani.
"Kifupi ni kwamba nimehangaika sana na mwanangu huyu, tangu akiwa mchanga mpaka leo, bahati mbaya ni kwamba baba yake mzazi alifariki mwaka 2007 na kuniachia mzigo ambao kwa hakika nimeuvumilia na kushindwa kujua mwishowe utakuwaje," alisema Grace.
Grace aliongeza alikuja jijini Dar mwezi uliopita kwa ajili ya matibabu ya mtoto wake huyo katika Hospitali ya Muhimbili, lakini aliambiwa arejee nyumbani na mwanaye akielezwa mwanae ni mlemavu wa ngozi mweusi (Albino Mweusi).
"Kama mtoto anavyokueleza, nawaomba wasamaria wema, serikali na watu wenye uwezo watusaidie.. wanichangie nimuokoe mwanangu...miaka 11 ya mateso nadhani inatosha, sitaki kumpoteza mwanangu nampenda katika hali aliyonayo," alisema Grace akilengwalengwa na machozi.
Alisema huyo ni mmoja wa watoto wake watatu aliozaa na mwanaume ambaye bahati mbaya hakufunga naye ndoa kabla ya kufa kwa ajali ya gari wakati wakiendelea kuhangaikia kwa pamoja matibabu ya Honolina.
"Huyu ni mtoto wangu wa kwanza kuzaa na Christian niliyezaa naye watoto watatu, wengine ni Dickson (9) na mwisho aliniacha nikiwa mjamzito wa mimba yake ni Francis (6), ambao wote hawana tatizo kama dada yao," alisema.
Alisema watoto wake hao kwa sasa wanaishi pekee yao Mgeta, Morogoro wakati yeye akihangaika na Honolina apate matibabu, akidokeza pia nyumba aliyokuwa amejenga na 'mumewe' imeuzwa na mama mkwe wake na hivyo kumfanya kuwa na wakati mgumu kwa vile ana pa kuishi na hana shughuli ili kumtibia mwanae.
Aliongeza kwa yeyote atakayeguswa na tatizo la mwanae anaweza kumsaidia kwa kuwasilisha michango yao ama kwa MZUKA WA FUNGO au kupitia simu zake za mkononi kwa huduma za Tigo-Pesa, M-Pesa au Airtel Money kwa namba 0719-749542, 0687-402694 na 0762-425973.
NB:Makala ndefu ya mtoto huyu itawajia baadaye kidogo, unaweza kulia kwa jinsi inavyosikitisha
Endelea Kusoma >>

RAIS ATEMBELEA UKUMBI WA BUNGE MJINI DODOMA LEO

0 comments
Rais Kikwete akizungumza na Naibu Spika Mhe Job Ndugai na Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashilila baada ya kutembeleaUkumbi wa Bunge mjini Dodoma leo



PICHA NA IKULU

 Rais Kikwete akikaribishwa kutembelea Jengo la Bunge mjini Dodoma na Naibu Spika Mhe. Job Ndugai leo

Rais Kikwete akitembelea Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo

Rais Kikwete akiangalia sehemu ya viti ndani ya Ukumbi wa  Bunge mjini Dodoma leo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Alhamisi, Oktoba 24, 2013 ametembelea na kukagua Jengo la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma kujionea maandalizi ya jinsi Wabunge wa Bunge Maalum la Katiba watakavyokaa katika Ukumbi wa Bunge hilo. Bunge hilo Maalum la Katiba litakuwa na Wabunge 600 tofauti ya Bunge la sasa lenye Wabunge 354 ambao ni pamoja na Wabunge 239 wa kuchaguliwa kutoka majimboni, Wabunge Wanawake Viti Maalumu 102, Wabunge wa kuteuliwa toka Baraza la Wawakilishi Zanzibar 5, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wabunge 7 (kati ya 10) wa kuteuliwa na Rais.
Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu