Monday, September 30, 2013

0 comments

FRANSIC MIYEYUSHO AMTWANGA SADIK MOMBA KWA POINT


Bondia Sadiki Momba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Miyeyusho wakati wa mpambano wao usiokuwa wa ubingwa uliofanyika siku ya jumapili katika ukumbi wa  Friends Coner  Manzese Dar es salaam Miyeyusho alishinda kwa pointi
Bondia Sadiki Momba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Miyeyusho wakati wa mpambano wao usiokuwa wa ubingwa uliofanyika siku ya jumapili katika ukumbi wa  Friends Coner  Manzese Dar es salaam Miyeyusho alishinda kwa pointi 
refarii Sako Mtlya akimnyoosha mkono juu bondia  Fransic Miyeyusho baada ya kumgalagaza Bondia Sadiki Momba wakati wa mpambano wao 
Bondia Mussa Sunga kushoto akipambana na Fahiri Awadhi wakati wa mpambano wao uliofganyika jumapili Awadhi alishinda kwa Point 
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi Nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akitoa maelezo ya DVD zake zenye mabambano ya ngumi makali kwa ajili ya kuangalia na kujifunza ngumi nzito zenye msisimko zinazofanyika duniani kote kocha huyo wa mchezo wa masumbwi alikuwa akionesha DVD za Lenox Lewis,Manny Paquaio,Mohamedi Ali,Floyd Mayweather, na wengine kibao 
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi Nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akitoa maelezo ya DVD zake zenye mabambano ya ngumi makali kwa ajili ya kuangalia na kujifunza ngumi nzito zenye msisimko zinazofanyika duniani kote kocha huyo wa mchezo wa masumbwi alikuwa akionesha DVD za Lenox Lewis,Manny Paquaio,Mohamedi Ali,Floyd Mayweather, na wengine kibao 
Baadhi ya raia wa kigeni kutoka china waliokuja kumsapoti bondia mussa sunga wakiwa katika picha ya pamoja na bondia huyo
DVD KALI ZA MCHEZO WA NGUMI ZINAZOSAMBAZWA NA KOCHA SUPER D
Mashabiki wa mchezo wa masumbwi picha zote na Super D Blog
Endelea Kusoma >>

Shule ya sekondari ya Weruweru washeherekea kitimiza miaka 50

0 comments
Baadhi ya akina mama waliosoma katika shule hiyo akiwa mama Asha Migiro wa kutoka kulia katika picha na wa sita kulia ni Oliver Baltazery

sisita akishangaa hat wewe imefika nashukuru sanauendelee kuwa na moyo huohuo

Basi ambalo nalo likiwa katika viwanja vya shule hiyo likisubiri waalikwa

picha halisi inaonyesha baadhi ya watu waliofika wakiwa nje ya mandhalui ya shule

picha inaonyesha nembo ya shule hiyo ambayo siku hiyo ilikuwa kiburudisho tosha kwenye vbazi la khanga lililokuwa vazi maalum kwa kila mtu alifika

watu waliserebuka katika muziki

Basi lililowachukua baadhi ya mbalimbali pamoja na wazazi waliokwenda katika sherehe hiyo

hivi ndivyo vibwagizo vya sherehe ya kutimiza miaka 50 ya sekondari ya Weruweru

Baadhi ya wanafunzi waliosoma katika  shule ya sekondari  ya WERUWERU Oliver Baltarzary wakiwa katika picha ya pozi wakati wa sherehe ya kutimiza miaka 50th Anniviversar picha zote na Oliver Baltazer

Endelea Kusoma >>

Sunday, September 29, 2013

0 comments
 Katiba ni Mwafaka wa Kitaifa. Viongozi zungumzeni
FROM Zitto Zuberi Kabwe TO 1 recipient
Show Details

From

        Zitto Zuberi Kabwe 

   
Katiba ni Mwafaka wa Kitaifa. Viongozi zungumzeni
by zittokabwe
Kwa takribani wiki tatu sasa kumekuwa na sintofahamu kuhusu muswada wa sheria uliopitishwa na Bunge ili kufanya marekebisho ya sheria ya marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011. Mjadala na upitishaji wa sheria hii uliweka rekodi ya pekee katika nchi yetu kwa vitendo vya kihuni kutokea Bungeni ambavyo nisingependa kuvirejea kutokana na aibu kubwa ambayo Bunge liliingia. Kiukweli kuna sintofahamu katika nchi kuhusu kuandikwa kwa Katiba mpya. Hii imechangiwa na kurushiana maneno miongoni mwa wanasiasa wa pande zote mbili, wanaopinga muswada ulivyo na wanaounga mkono muswada ulivyo. Masuala ya Tume imalize kazi yake lini, ushiriki wa Zanzibar na idadi ya wajumbe kutoka Zanzibar kwenye Bunge la Katiba, Wajumbe wa Bunge Maalumu wanapatikanaje na kadhalika ni masuala ambayo yanaweza kupatiwa mwafaka kwa viongozi kukaa na kuzungumza. Haya sio masuala ya kushindwa kujenga mwafaka labda kuwe na nia mbaya dhidi ya mchakato wa kuandika Katiba mpya. Katiba sio suala la kufanyia siasa. Katiba ni uhai wa Taifa.
Ni wazi kuna kundi kubwa ambalo halijitokezi waziwazi ambalo lingependa pasiwe na katiba mpya ya Wananchi. Kuna kundi lingine ambalo lingependa mchakato wa kuandika Katiba uendelee kwa miaka mingine zaidi ili kuweza kupata Katiba bora. Kuna kundi la Wabunge ambao kwa chinichini wanataka mchakato uendelee, uchaguzi uahirishwe mpaka mwaka 2017 na wao waendelee kuwa wabunge. Naamini watu hawa wanaota ndoto za mchana kwani hakuna mahusiano yeyote kati ya uchaguzi mkuu na kuandika katiba mpya. Kama Bunge hili la sasa na Serikali hii itashindwa kukamilisha zoezi hili, Bunge linalokuja na Serikali itakayoingia madarakani itaendelea nalo. Hivyo sio lazima kupata Katiba mpya kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015. CHADEMA imependekeza kuwepo na marekebisho ya mpito kwenye Katiba ya sasa ili kuwezesha Tume huru ya Uchaguzi, masuala ya wagombea binafsi na kadhalika. Vyama vingine vya siasa vinaweza kuwa na mapendekezo yao ya mpito na hivyo kutoa nafasi ya kutosha kabisa wa kuandika Katiba makini.
Changamoto kubwa sana ya siasa za Tanzania ni kelele. Wanasiasa hatuzungumzi kwenye masuala yanayohusu uhai wa Taifa. Kila chama kinakuwa na misimamo yake na kuishikilia na hatimaye kujikuta tunapoteza fursa ya kuzungumza na kujadiliana kama Watanzania. Mwaka 2011 hali ilikuwa hivi hivi mpaka kundi la Wazee viongozi wastaafu walipoingilia kati na kupelekea wanasiasa kukaa na kuzungumza. Bahati mbaya sana viongozi wale ndio sasa wamepewa usukani wa kuandika Katiba kwa kuwa kwenye Tume. Hawawezi tena kufanya kazi ile ya kutafuta suluhu iliyopelekea Rais kuzungumza na viongozi wa vyama vyote vya siasa ikulu jijini Dar es Salaam.
Vyama vya Upinzani nchini sasa vimeungana kupinga muswada wa marekebisho ya Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011. Waziri wa Sheria na Katiba, Waziri wa Nchi ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu, viongozi waandamizi wa CCM wote nao wameungana kuunga mkono muswada kama ulivyo. Badala ya kutafuta mwafaka, kumekuwa na kurushiana maneno ya kejeli na kadhalika. Taifa halijengwi namna hii. Taifa linajengwa kwa mwafaka na Katiba ni moja ya nyenzo wa Mwafaka wa Taifa. Niliwahi kuandika huko nyuma kuwa Katiba haiandikwi barabarani bali huandikwa mezani kwa watu kukaa na kukubaliana masuala ya Taifa dhidi ya maslahi ya kivyama ya wanasiasa.
Hakuna kilichoharibika. Bado tunayo nafasi kama Taifa kukaa na kukubaliana. Kwa hali ya sasa nafasi hii ipo mikononi mwa Mkuu wa Nchi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Rais ana wajibu wa kikatiba wa kuhakikisha umoja wa kitaifa unaendelea kuongoza mchakato huu wa katiba ya nchi yetu. Hata hivyo ni vizuri kutahadharisha kuwa sio sahihi kwa wanasiasa wa pande zote kujaribu kumlazimisha Rais kuridhia ama kutoridhia sheria hiyo. Si sawa kisiasa kwa wanasiasa wa upinzani kujaribu kumlazimisha Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama chenye wabunge wengi bungeni kwenda tofauti na wabunge wake na wakati huohuo ni utovu wa nidhamu kwa Waziri wa Sheria kujaribu kumshauri hadharani Rais wake kuridhia sheria hiyo kwani ni kinyume cha misingi ya uongozi na pia kinatafsirika kama kumshurutisha (blackmail) Rais wake.
Kutosaini muswada huu kunaweza kuleta mgongano kati ya Wabunge wa CCM na Rais. Hata hivyo Rais lazima aweze kushawishi chama chake kwamba umoja wa kitaifa ni muhimu ziadi kuliko maslahi ya kisiasa ya chama chao. Pia kikatiba Rais anasaini miswada kuwa sheria akiwa Mkuu wa Nchi na sio Mkuu wa Serikali ya Jamhuri. Akiwa Mkuu wa Nchi maslahi mapana ni kuweka mwafaka wa pamoja miongoni mwa wananchi. Rais Jakaya Kikwete anapaswa kutumia mamlaka yake kama Mkuu wa Nchi kuiweka nchi pamoja kwa kuurejesha muswada bungeni ili uweze kujadiliwa upya na wadau wote na kupitishwa tena na Bunge. Ibara ya 97 ya Katiba ya sasa imeweka masharti ya utaratibu wa kutunga sheria na iwapo Rais ataurudisha muswada huu Bungeni pamoja na maelezo ya hatua hii, upitishwaji wake utahitaji theluthi mbili ya wabunge wote. Hii itakuwa hatua muhimu sana katika historia ya demokrasia yetu. Rais afuate ushauri huu kwani una manufaa makubwa.
Hata hivyo, ni lazima pawepo na mazungumzo miongoni mwa wanasiasa na makundi ya kijamii kuhusu Katiba. Katiba nzuri itapatikana pale tu ambapo mazingira ya kisiasa yanaonyesha nia njema kwa pande zote kisiasa. Kukwepa kuangaliana machoni na kuzungumza tofauti zetu za kimitazamo ni hatari zaidi. Juzi ngumi zimerushwa Bungeni. Kesho zitakua mitaani na vijijini kwetu. Tunataka kujenga Taifa la namna hiyo?
zittokabwe | September 28, 2013 at 3:28 PM | Tags: CCM, Chadema, katiba, Rais, Upinzani, zanzibar | Categories: Tanzania, Zitto Kabwe | URL: http://wp.me/pRboX-Nu
Endelea Kusoma >>
0 comments





 
Tutakomesha tatizo la watu kumwagiwa tindikali - JK

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kuwa Serikali yake imedhamiria na itahahakisha kuwa inalimaliza balaa la watu kumwagiwa tindikali iwe ni Zanzibar ama Tanzania Visiwani.

Hata hivyo, Rais Kikwete amesema kuwa katika siku za karibuni Jeshi la Polisi lilifanya operesheni kubwa katika mitaa ya Zanzibar ambako watu 10 wametiwa mbaroni kwa tuhuma za kushiriki mipango ya kuandaa na kutekeleza vitendo hivyo.

Rais amemwambia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Mheshimiwa Ban Ki Moon kuwa chimbuko la tatizo hilo lina sura nyingi lakini hakuna shaka kuwa katika kipindi kifupi iwezekanavyo Serikali itafikisha tatizo hilo mwisho wake.

Rais Kikwete ametoa msimamo huo wa Serikali kuhusu vitendo ambavyo vimekuwa vinaongezeka vya watu mbali kushambuliwa kwa kumwagiwa tindikali, tatizo ambalo kimsingi lilitokea kwa mara ya kwanza Zanzibar wakati kiongozi maarufu wa Kiislamu Sheikh Soroga alipomwagiwa tindikali akifanya mazoezi ya viungo asubuhi moja kwenye mitaa ya mji wa Unguja.

Rais Kikwete ametoa msimamo huo wakati alipokuwa anazungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ofisini kwake mjini New York, Marekani, leo, Ijumaa, Septemba 27, 2013 baada ya kuwa ameulizwa jambo hilo na Mheshimiwa Ban Ki Moon kuhusu tatizo hilo.

Ni kweli tumekuwa na vitendo hivyo, zaidi Visiwani Zanzibar kuliko Bara ambako hata hivyo nako vimekuwepo vitendo hivyo. Ni jambo la kulaaniwa sana na karibuni Jeshi la Polisi lilifanya operesheni maalum na msako mkubwa Tanzania Visiwani ambako watu 10 wametiwa mbaroni na watafikishwa katika vyombo vya sheria.”

Amesisitiza Rais Kikwete: “Wakati lilipoanza tatizo hilo, tulidhani kuwa alikuwa ni Sheikh Soroga aliyekuwa anatafutwa peke yake na watu ambao walikuwa hawakubaliani kisiasa na msimamo wake,lakini mara wakaanza kushambuliwa watu wengine wakiwemo wasichana wawili wa Uingereza ambao walikuwa wanafanya kazi za kujitolea tu. Tatizo hili ni lazima likome.”

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

Endelea Kusoma >>

Saturday, September 28, 2013

MREKING NEWZZZZ

0 comments
SERIKALI IMEYAFUNGIA MAGAZETI MAWILI  MWANANCHI NA MTANZANIA MAGAZETI HAYO MTANZANIA LIMEFUNGIWA KWA SIKU 90 NA MWANANCHI LIMEFUNGIWA KWA SIKU 14 HABARI KAMILI TUTAWALETEA
Endelea Kusoma >>

Friday, September 27, 2013

WASHITAKIWA WA EPA WAHUKUMIWA KWENDA GEREZANI

0 comments
MSHITAKIWA  EDDAH MWAKALE NA BAHATI MAHENGE WAKITEREMKA KUTOKA KATIKA MAHAKAMA AYA KISUTU  MARA BAADA YA KUTOLEWA HUKUMU YA KUPELEKWA GEREZANI KWA KOSA  FEDHA ZA EPA LEO

Washitakiwa kesi ya Epa toka kushoto ni Bahati Mahenge, Manase Mwakale na  Eddah Mwakale wakiwa katika mahakama ya kisutu kusomewa shitaka lao na kufungwa jela

Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo kwenye ofisi za ubalozi wa Kenya wa kudumu katika Umoja wa Mataifa jijini New York jana kufuatia shambulizi la kigaidi katika sehemu ya biashara ya West Gate jijini Nairobi Kenya hivi karibuni.Kulia ni Naibu Balozi wa Kenya wa kudumu Umoja wa Mataifa(Deputy Permanent Representative) Mhe.Koki Muli Grignon PICHA NA FREDY MARO WA IKULU

 Luteni Jenerali Sylvester Rioba akipunga mkono wakati akiwa katika gari malumu la kijeshi ambalo hutumiwa  katikasherehe za kuaga maofisa wenyengazi za majenerali sherehe hizo zimefanyika katika kambi ya  Abdala Twalipo Dar re salaam  picha na chris mfinanga

MANASE MWAKALE AKIWA NA BAHATI MAHENGE  WAKIPELEKWA MAHABUSU LEO KATIKA MAHAKAMA AYA KISUTU MARA BAADA YA KUSOMEWA SHITAKA LAO LA UPOTEVU WA FEDHA ZA EPA

Endelea Kusoma >>
0 comments
 KUTOKA KAPITALI ONLINE MARKETING & ADVERTISING COMPANY INAWALETEA BLOG HII MAALUM KWA AJILI YA MUSIC WA BONGO TU ,LIVE SHOW ZA WASANII WA BONGO NA INTERVIEW ZAO
UKITEMBELEA BLOG HII UTAWEZA KUPATA VIDEO ZOTE KALI ZA BONGO
NA MATUKIO YANAYOHUSU WASANII KWA VIDEO
...KWA WASANII WANAOHITAJI VIDEO ZAO ZIWEKWE KWENYE HII BLOG WANAWEZA WASILIANA NASI KWA
EMAIL: videozabongo@gmail.com
PIA TUNAFANYA VIDEO PROMOTION

KUTOKA:
FOUNDER ,ERICK KISAI
KAPITALI ONLINE MARKETING & PROMOTION COMPANY
DAR ES SALAAM.

ANGALIA VIDEO HIZI
ANGALIA VIDEO HIZI MPYA KABISA
Endelea Kusoma >>

MAKAMU WA KWANZA WA RAIS ZANZIBAR ATEMBELEA TANGA NA DAR

0 comments
 Baadhi ya Wazanzibari wanaoishi Tanga wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad katika ukumbi wa Tangamano jijini Tanga, leo  (picha na Salmin Said, OMKR)

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akiwapungia mkono wananchi wakati akitoka katika ukumbi wa hoteli ya Starlight jijini Dar es Salaam, baada ya kuzungumza na Wazanzibari wanaoishi Dar es Salaam.jana (picha ya Salmin Said, OMKR.

 Baadhi ya Wazanzibari wanaoishi Tanga wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad katika ukumbi wa Tangamano jijini Tanga, LEO



DAR ES SALAAM      NA TANGA                               
Wazanzibari wamehimizwa kuitumia vyema fursa ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, ili waweze kushiriki katika maamuzi yanayohusu nchi yao.
Wito huo umetolewa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, alipokuwa akizungumza na Wazanzibari wanaoishi Dar es Salaam katika mkutano uliofanyika hoteli ya Starlight jijini Dar es Salaam.
Amesema wakati mchakato wa kulifanyia uhakiki daftari la kudumu la wapiga kura kwa kuandikisha wapiga kura wapya  ukiendelea Zanzibar, bado kuna idadi ndogo ya wanaojitokeza kujiandikisha ikinganishwa na tathmini ya Tume ya Uchaguzi.
Amesema ili kuhakikisha kuwa wananchi wanashiriki katika maamuzi yanayohusu Zanzibar likiwemo suala la kura ya maoni kwa ajili ya kupitisha au kukataa katiba mpya, hawana budi kujiandikisha katika daftari la kudumu ili waweze kuitumia haki hiyo ya kupiga kura.
Ametoa wito kwa wananchi wenye sifa kujiandikisha katika  daftari la kudumu la wapiga kura, ili waweze kuitumia haki yao hiyo ya kidemokrasia.
Akizungumzia kuhusu mchakato wa kuandika katiba mpya ya Tanzania, Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF amesema bado hajaridhishwa na baadhi ya vipengele vilivyomo katika mswada wa sheria inayohusu marekebisho ya Katiba, ambapo Serikali pamoja na asasi za kiraia Zanzibar hazikushirikishwa katika marekebisho hayo.
Amesema katiba ni jambo kubwa linaloeleza mustakbali wa taifa kwa kipindi kirefu, hivyo kufikia pahala ikapitishwa kwa ushindi mdogo (just simple majority), halitokuwa jambo la busara kwa mustakbali wa Taifa.
Amefahamisha kuwa wakati mchakato huo wa katiba ukiendelea ni vyema kwa washirika wa Muungano kuwa na fursa sawa kama nchi, hasa katika ushiriki wa wajumbe kwenye Bunge la Katiba.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Jimbo la Ole (CUF), Hamad Massoud Hamad amesema takwimu za uandikishaji katika daftari hilo ambao umekamilika kwa upande wa Unguja zinaonesha kuwa idadi kubwa ya wananchi hawakujitokeza katika uandikishaji huo.
Amedai kuwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ilitarajia kuandikisha zaidi ya wapiga kura laki moja kwa Wilaya sita za Unguja, lakini hadi zoezi hilo linakamilika ni asilimia 23 ya wananchi waliojitokeza kuandikishwa.
Wakati zoezi hilo likikamilika kwa upande wa Unguja, linatarajiwa kuanza rasmi katika Wilaya nne za Pemba ambapo watu wapatao 52 elfu wanatarajiwa kusajiliwa.
Zoezi hilo litakaloanzia Wilaya ya Micheweni tarehe 12/10/2013, litakuwa likifanyika siku tatu kwa kila shehia.
Amewasisitiza wananchi wenye sifa kutopuuza fursa hiyo, kwani kuwa na Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi (ZAN ID) na kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, ni fursa za kipekee katika kushiriki masuala ya kitaifa na maendeleo kwa ujumla.
Mapema akisoma risala ya Jumuiya ya Wazanzibari wanaoishi Tanzania Bara, Said Rashid Salum amesema watashirikiana na wazanzibari popote walipo katika kutetea haki na maslahi ya Zanzibar katika Nyanja zote za kimaendeleo.
Mkutano kama huo unatarajiwa kufanyika katika Mkoa wa Tanga, tarehe 27/09/2013.

Hassan Hamad (OMKR).

Endelea Kusoma >>
0 comments
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba akizungumza na wadau  wanaohusika na sekta ya usafirishaji majini wakati wa kongamano la kuadhimisha siku ya Bahari Duniani lililofanyika jijini Mwanza hivi karibuni.


Endelea Kusoma >>

Thursday, September 26, 2013

0 comments

KARAMA NYILAWILA KUZIPIGA OCTOBA 20


Karama Nyilawila
BONDIAw a ngumi za kulipwa nchini, Karama Nyilawila aliyewahi kuwa bingwa wa dunia wa WBF uzito wa middle anatarajiwa kupanda ulingoni mwezi ujao kuzipiga na Sado Philemon.
Nyilawila aliyempiga Kreshnik Qato wa Czech wakati akitwaa taji lake la WBF ambalo alilitema baada ya kushindwa kwenda kulitetea ili apate nafasi ya kuzipiga kirafiki na Francis Cheka mjini Morogoro na kudundwa, atazipiga na Philemon kwenye ukumbi wa CCM Mwinjuma siku ya Oktoba 20, pambano lililoandaliwa na kampuni ya Bigright Promotion.
Mratibu wa pambano hilo, Ibrahim kamwe alisema kuwa maandalizi mpaka sasa yanaenda vizuri.
Hata hivyo Kamwe alisema mabondia wanaendelea kujifua kimkandamkanda kutokana na kukosekana kwa wadhamini na hasa mabondia watakaosindikiza pambano hilo.
Kamwe alisema Nyilawila na mwenzake wameshasaini makubaliano ya kupanda ulingoni siku hiyo ambapo watasindikizwa na michezo kadhaa itakayohusisha mabondia chipukizi.
Endelea Kusoma >>

MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM

0 comments











TANZANIA FOOTBALL FEDERATION
VODACOM PREMIER LEAGUE (VPL) 2013/2014










NO TEAMS P W D L GF GA GD PTS
1 Simba SC 5 3 2 0 13 4 9 11
2 JKT Ruvu FC 5 3 0 2 6 2 4 9
3 Azam FC 5 2 3 0 8 5 3 9
4 Ruvu Shooting FC 5 3 0 2 6 3 3 9
5 Coastal Union FC 5 2 3 0 4 1 3 9
6 Kagera Sugar FC 5 2 2 1 6 3 3 8
7 Mbeya City SC 5 1 4 0 5 4 1 7
8 Young Africans SC 5 1 3 1 10 7 3 6
9 Mtibwa Sugar FC 5 1 3 1 3 4 -1 6
10 Rhino Rangers FC 5 0 4 1 5 7 -2 4
11 JKT Oljoro FC 5 1 1 3 3 6 -3 4
12 Mgambo Shooting FC 5 1 1 3 2 10 -8 4
13 Tanzania Prisons FC 5 0 3 2 2 8 -6 3
14 Ashanti United SC 5 0 1 4 2 11 -9 1

TOTAL 35 10 15 10 75 75 0 90

AS FOR: 22/09/2014








Endelea Kusoma >>
0 comments

SIMBA SPORTS CLUB            
P.O.BOX 15318 | TEL+255 222183330 |FAX +255 222183330 |MSIMBAZI/MCHIKICHI STREET | DAR ES SALAAM | TANZANIA | EMAIL   simbasportsclub@yahoo.com|WEBSITE www.simba.co.tz| AFFILIATED TO TFF, DRFA and IDFA

                                                                                                     

KLABU ya Simba inapenda kutoa taarifa zifuatazo kwa umma kuhusu masuala yanayoihusu kwa sasa.

Kuhusu Emmanuel Okwi

KATIKA siku za karibuni, vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini vimeripoti kuhusu uwepo nchini wa aliyekuwa mchezaji wa zamani wa klabu, Emmanuel Arnold Okwi kutoka nchini Uganda.

Taarifa hizo zimeeleza mambo mbalimbali ikiwamo taarifa kuwa Simba Sports Club ina mawasiliano na mchezaji huyo na alikuja kwa mwaliko wa viongozi wa klabu. Baadhi ya vyombo vimekwenda mbali zaidi na kudai kuwa uongozi wa Simba unamshawishi mchezaji huyo avunje mkataba wake na klabu anayoichezea sasa ya Etoile du Sahel  (ESS) ya Tunisia.

Klabu inapenda kuuarifu umma kwamba Simba au kiongozi wake yeyote (Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Wajumbe wa Kamati ya Utendaji na Sekretarieti haijahusika kwa namna yoyote ile na ujio wa mchezaji huyo hapa nchini. Hakukuwepo na mwaliko rasmi au usio rasmi kwa viongozi wa Simba.

Taarifa zozote za kuhusisha ujio wa Okwi na uongozi wa Simba ni za upotoshaji na zina lengo la kuharibu heshima na hadhi ambayo uongozi huu umeijenga kitaifa na kimataifa kwenye tasnia ya soka.

Hata hivyo, kisheria, Simba haiwezi kumzuia mchezaji huyo kusafiri kwenda nchi yoyote anayotaka kama amefuata sheria zote za uhamiaji. Mchezaji huyo ana mkataba na timu nyingine na Simba haihusiki na safari zake, matembezi yake au mipango yake ya kimaisha.

Uongozi wa Simba unafahamu kwamba Okwi ni mchezaji halali wa ESS maana wenyewe ndiyo uliomuuza kwa klabu hiyo. Kwa mujibu wa sheria za FIFA, klabu yeyote, ikiwamo Simba SC, haziruhusiwi kufanya mawasiliano na mchezaji huyo au yeyote yule halali wa klabu nyingine bila ruhusa ya klabu yake kama mkataba wa mchezaji husika umebakiza kipindi kinachozidi miezi sita. Hii maana yake ni kwamba uongozi hauwezi kumshawishi mchezaji huyo kujiunga na klabu.

Ikumbukwe kwamba hadi sasa, klabu ya Simba, inaidai klabu ya Etoile du Sahel kiasi cha dola za Marekani 300,000 (laki tatu) ambazo zinapaswa kuwa zimelipwa kabla ya tarehe 30 mwezi huu wa tisa mwaka 2013. Kinyume cha hapo matokeo mengine yataamuliwa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya FIFA ambapo makubaliano husika yalisajiliwa.

Uongozi wa Simba ungeomba vyombo vya habari na watu binafsi waache kutoa taarifa zozote za kuhusisha ujio wa Okwi na klabu au kwamba kuna mipango ya kumshawishi avunje mkataba wake kwani taarifa hizo hazina ukweli wowote.

Imetolewa na

Ezekiel Kamwaga,
Ofisa Habari,
Simba Sports Club


Endelea Kusoma >>

BREAKING NEWS !!!! MWANDISHI WA MWANACHI AFARIKI DUNIA LEO

0 comments
Mwandishi wa habari wa kampuni ya Mwanchi Communication Limited mkoa wa Morogoro, Venance George (Pichani anayeangalia kamera) amefariki dunia katika  JUMA MTANDA BLOG...

Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu