Thursday, July 31, 2014

VIONGOZI WA UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI (UKAWA)WATOA TAMKO LA LAO KUHUSU WITO ULIOTOLEWA NA VIONGOZI WA DINI KUWATAKA WAREJEE BUNGENI

0 comments
Viongozi wakuu wa Umija wa katiba ya wananchi (UKAWA) wakishikana mikono kuashiria umoja mara baada ya kuongea na wandishi wa habari kutoa Tamko la Ukawa kuhusu Wito wa Viongozi wa Dini wa kurudi Bungeni kutoka kulia ni profesa Sfari katibu mkuu wa NCCR mageuzi Mosena Nyambabe ,mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe ,Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba,Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi Jaqmes Mbatia na katibu mkuu wa Chadema Wilbrod Slaa , mbunge sakaya na Itatiro wakiwa nje ya makao makuu ya cuf

viongozi wa ukawa kulia ni mwenykiti wa umoja wa katiba ya wananchi ukawa profes Ibrahim Lipumba na mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowewakitoka katika ofisi kuu ya cuf wakielekea katika chumba cha mkutano tayari kuongea na wandishi wa habari kuhusu tamko lao kuhusu viongozi wa dini kuwataka warejee bungeni

Mwenyekiti wa Umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) Profesa Ibrahim Lipumba (katika)akisisitiza jambo wakati akiongea na wandishi wa habar kutoa Tamko kuhusu Wito wa Viongozi wa Dini wa kurudi Bungeni kushoto ni mwenyekiti awa Chadema Freeman Mbowe na kulia ni Mwenyeti wa NCCR mageuzi James Mbatia

Endelea Kusoma >>

Wednesday, July 30, 2014

BREKING NEWZZZZZZ WATU 17 WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

0 comments
 watu wapatao 17 wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya basi la moro best na lorikugongana uso kwa uso katika eneo la panda mbili mkoani dodoma leo basi hjilo la moro best lilikuwa lkinatoka mpwapwa na kuelekea Dar es salaam baadhi ya washuhuda ya ajali hiyo wanaseema lori hilo lilikuwa katika mwendo kasi wakati akilipita basi hilo madereva wa magari yote wamefariki papohapo pamoja na iutingo

Basi la  Morobest lenye na namba za usajili T 258
AHV lilipopata jali ya kugongana uso kwa uso na Lori
  na kuua Watu 17 katika eneo la Pandambili
Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma ,Basi  liliokuwa likitoka Mpwapwa kwenda
Dar es salaam

Basi la  Morobest lenye na namba za usajili T 258
AHV lilipopata jali ya kugongana uso kwa uso na Lori
  na kuua Watu 17 katika eneo la Pandambili
Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma ,Basi  liliokuwa likitoka Mpwapwa kwenda
Dar es salaam

 


Lori lenye namba za usajili T 820 CKU na tela yenye namba za usajili T
390 CKT liliokuwa likiendeshwa na Dereva wake Gilbart Lemanya na Tingo
wake Mikidadi Zubery Omary  ambao wote walifariki papo hapo
linavyoonekana baada ya kugongana uso kwa uso na basi la Morobest
katika eneo la Pandambili Wilayani Kongwa  Mkoani Dodoma na

Endelea Kusoma >>

BREKING NEWZZZZ WATU 17 WAMEFARIKI DUNIA NA WENGINE WAMEJERUHIWA

0 comments
Abiaria wapatao 17 wamefariki dunia papohapo wengine kadhaa wamejeruhiwa baada ya basi la Moro Best lililokuwa likitokea mpwapwa kuelekea Dar essalaam kugongana uso kwa uso na Lori la Mizigo  katika eneo la Panda Mbili Dodoma ajali hiyo mbaya ilitokea leo habari zinasema ajali hiyo imetokea baada ya dereva wa lori kutaka kulipita lori jingine kutokana mwendo kasi ndipo ilipogongana usoso na maderevawsoto wa wili wamefariki papo hapo
Endelea Kusoma >>

Tuesday, July 29, 2014

SALA YA IDD FITRI IMEADHIMISHWA LEO

0 comments
baadhi ya mabalozi wakiwa katika sala ya idd

waumini wakiwa katika ibada ya sala ya idd

baadhi ya waumini wa kiioslama wakisalimia Rais wa zanzibar Dr  Ali Mohamed Shen

waumini wa kiislama wakiwa kwenye sala ya Iddi mjini dodoma leo

rais jakaya kikwete akisalimiana na waumini wa dini ya kiislama mara baada ya sala ya Idd iliyoadhimishwa leo

Rais jakaya kikwete akisalimiana nawatoto pamoja na waumini wa kiislama mara baada sala ya Idd leo

Rais jakaya kikwete akisalimiana na waumini wa kiislama mara baada sala ya Idd leo 

Endelea Kusoma >>

Monday, July 28, 2014

KUSITISHWA KWA AJIRA ZA KONSTEBO NA KOPLO WA UHAMIAJI

0 comments

Endelea Kusoma >>

WATUHUMIWA WA KESI YA HOSPITALI YA IMTU YA KUTUPA MIILI YA BINADAMU KATIKA MACHIMBO YA KUNDUCHI WAKIWA KATIKA MAHAKAMA YA KINONDONI LEO

0 comments
Watuhumiwa wa kesi  inayowakabili viongozi wa hospitali ya IMTU  watuhumiwa hao walifikishwa mahakama ya kinondoni kwa shitaka la kushindwa kufukia viungo vya binadamu vilivyotupwa kwenye machimbo ya kunduchi ambayo viungo hivyo vilitupwa hovyo ambavyo jumla ya viungo ni 83  kesi hiyo imefutwa na watuhumiwa kurudishwa tena polisi ili wafunguliwe mashitaka tena kwa picha wakiwa katika mahakama ya kinondoni


watuhumiwa wa IMTU  wakitoka katika mahakama ya kinondoni kuelekea kupanda difenda  kuelekea polisi  ambao wanadaiwa kutupa viungo vya binadam na kutovifukia vilivyokutwa katika machimbo ya kunduchi

watuhumiwa  wa IMTU wakipanda gari la polisi baada ya kesi yao inayodaiwa kutupa viungo vya binadamu bila kufukia katika machimbo ya kunduchikesi

watuhumiwa wakisindikizwa na poli katika mahakama ya kinondoni kesi ya inayowakabili ya kutofukia miili ya binadamu iliyotupwa katika machimbo ya kunduchihivi karibuni


Endelea Kusoma >>

WAISALAM WA ANSALI SUNA WASALI IDD

0 comments
baadhi ya waislam wa answal suna wakiwa kati sala ya idd leo iliyofanyika katika viwanja vya jangwani




Endelea Kusoma >>

Saturday, July 26, 2014

0 comments

*KATIBU WA BUNGE MAALUM AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI

 Katibu wa Bunge Maalum la Katiba, Yahaya Khamis  akizungumza na waandishi wa habari  leo (hawapo pichani ) kuhusu  kuendelea kwa  Bunge Maalum la Katiba kwa niaba ya Mwenyekiti  wa Bunge hilo, Samuel Sitta   katika ukumbi wa mikutano  wa ofisi ndogo za Bunge  jijini  Dares Salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza  Katibu wa Bunge Maalum la Katiba, Yahaya Khamis  akizungumza na waandishi wa habari  leo (hawapo pichani ) kuhusu  kuendelea kwa  Bunge Maalum la Katiba kwa niaba ya Mwenyekiti  wa Bunge hilo, Samuel Sitta   katika ukumbi wa mikutano  wa ofisi ndogo za Bunge  jijini  Dares Salaam. Picha na Magreth Kinabo - MAELEZO
****************************************
*SITTA - BUNGE MAALUM LA KATIBA KUENDELEA
Na Winner Abraham na Rose Masaka-MAELEZO-Dar es salaam
Mwenyekiti  wa Bunge Maalum la Katiba Samuel Sitta, amesema kuwa  Mkutano wa Bunge hilo, utaendelea kama ulivyopangwa  Agosti 5, mwaka huu mjini Dodoma.

Amesema kuwa licha ya baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo, kuendelea na msimamo wao wa kutaka kususia vikao vitakavyoanza mapema mwezi ujao, lakini bado kuna mambo muhimu ya kujadiliwa.

Mwenyekiti huyo ametoa kauli hiyo leo mjini Dar es salaam, katika taarifa yake iliyosomwa kwa niaba yake na Katibu wa Bunge Maalum la Katiba, Yahaya Khamis wakati wa mkutano wa waandishi wa habari.

 “Kamati hiyo, imeamua  kupendekeza kwa Kamati ya Uongozi kwamba  Bunge Maalum la Katiba liendelee  kwa  sababu  yapo masuala mengi muhimu ya kikatiba ambayo yanatuunganisha kama vile usawa wa kijinsia katika nafasi za uongozi na kuikarabati Tume ya  Taifa ya Uchaguzi(NEC).

 “Mambo mengine ni kurekebisha kikatiba masuala ya Muungano,haki za wakulima,wafugaji,wasanii na makundi mengineyo na ukomo wa vipindi vya uongozi,”alisema Sitta katika taarifa hiyo.

 Aidha  aliongeza kwamba uamuazi huo, umefikiwa baada ya wajumbe wa Kamati hiyo waliohuduria ambao walikuwa  zaidi ya theluthi  mbili   ya wajumbe wote, ambapo waliendelea na kikao.

Alisema  hatua ya baadhi ya wajumbe kwenda kwa wananchi na maoni yao imekuwa siyo muafaka na si wakati wake, hivyo Bunge hilo liwajibike katika siku za usoni kujibu upotoshwaji wowote kuhusu mchakato wa katiba kadri unavyojitokeza.

 Aliongeza kwamba Kamati hiyo, inaona  kwamba kwa kuendelea kulisusia Bunge hilo, na kupuuza wito wa jamii kupitia makundi mbalimbali pamoja na madhehebu ya dini inatilia shaka dhamira halisi  ya viongozi wa kundi hili la wasusiaji kupuuzia juhudi zote za usuluhishi, kunazua mashaka kuhusu lengo la ususiaji  kwamba pengine agenda ya viongozi hawa ni nyingine na siyo upatikanaji wa Katiba.

 Alisema Kamati hiyo inarejea kwamba  wajumbe hao  629 wamekabidhiwa jukumu adhimu na la kihistoria kwa niaba ya Watanzania jukumu ambalo hutokea baada ya miongo kadhaa ya uhai wa Taifa lolote.

“ Tutakuwa hatuwatendei haki Watanzania ikiwa hatutafikia maridhiano yanayotuwezesha kukamilisha kazi tuliyopewa,” alisisitiza.

 Mwenyekiti huyo alisema katika ngwe ya pili inayoanza mapema mwezi ujao mkutano wa Bunge hilo,  uzingatie upya baadhi ya Kanuni za Bunge hilo, ambazo ni kikwazo katika kuhakikisha kwamba kazi ya kujadili na hatimaye  inayopendekezwa inakamilika ndani ya siku 63 zilizosalia kisheria, kati ya hizo siku 60 ni za nyongeza na tatu  zilizokuwa pungufu za siku 70 za awali.

 Alisema Kamati hiyo, inaendelea kutoa wito wa wajumbe waliosusia mikutano ya Bunge hilo, kurejea katika Bunge hilo, ambalo pekee ndiyo lina uwezo wa kisheria wa kutatua matatizo yaliyopo.

Amesema kuwa kwa mujibu wa Kanuni ya 54 kifungu cha nne na tano ya Kanuni za Bunge Maalum la Katiba, aliteua Kamati ya Mashauriano ya wajumbe thelathini (30) kujadili matatizo yaliyojitokeza Dodoma katika mkutano ulipita lakini wajumbe kutoka Chama cha CUF, CHADEMA na NCCR Mageuzi,walikisusa kikao cha jana Julai 24 mwaka huu.

“Jitihada mbalimbali zilizofanywa na sekretarieti pamoja na mwenyekiti  hadi  asubuhi ya siku ya mkutano hazikuweza kuwashawishi wajumbe hao wasusiaji kuhudhuria kikao, alisema  Sitta  katika taarifa yake.  

Aliitaja athari za kutoendelea na mchakato uliopangwa wa kuandaa na hatimaye  kuipigia kura Katiba mpya  ni pamoja na  kupoteza mabilioni ya fedha  za wananchi zilizokwisha tumika katika kazi, baya zaidi ni kuiweka rehani amani ya nchi yetu kwa kuukuza mno  mgogoro wa katiba na kuwagawa wananchi kwa propaganda hadi uchaguzi mkuu 2015.
Endelea Kusoma >>

RAIS JAKAYA KIKWETE AHUDHURIA MAHAFALI YA KOZI YA PILI YA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI TAASISI MALUUM UTOAJI MAFUNZO YA USALAMA WA KITAIFA NA KIMATAIFA

0 comments
Profesa ibrahim lipumba akisalimiana na mkuu wa majeshi ya ulinzi  David Mwamunyange wakati wa mahafali ya pili ya chuo cha jeshi  NDC

MKUU WA JESHI LA POLISI  MANGU AKIWA NA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM MECK SADIK

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIONGEA NA WAKUU WA JESHI LA POLISI NA MAGEREZA

RAIS JAKAYA KIKWETE AKISALIMIANA NA ERNEST WAMBA DIA WAMBA

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIFURAHIA JAMBO PAMOJA NA DR BANA NA PROFESA IBRAHIM LIPUMBA
WAHITIMUWA JESHI




RAIS JAKAYA KIKWETE AKIWA NA WAHITIMU WA MAHAFALI

RAIS AKIWA NA WATU MBALIMBALI

WAHITIMU WA CHUO CHA JESHI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA

RAIS JAKAY KIKWETE AKIELEKEA KATIKA JUKWAA

RAIS AKIONGEA NA BAADHI YA MABALOZI

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIAGANA WAKUU WA JESHI LA ULINZI

RAIS JAKAY KIKWETE AKIELEKEA KATIKA JUKWAA 

BAADHI YA WANAJESHI WAHITIMU KATIKA CHUO CHA JESHI WAKATI WA MAHAFALI YA PILI YA CHUO HICHO

BAADHI YA WANAJESHI WAHITIMU KATIKA CHUO CHA JESHI WAKATI WA MAHAFALI YA PILI YA CHUO HICHO 

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIWAAGA WAHITIMU WANAJESHI WA CHUO CHA JESHI LEO

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIFURAHI KITUPAMOJA NA WAGENI MBALIMBALI

Endelea Kusoma >>
0 comments

SHIWATA yaipongeza Serikali kutambua kijiji chao Mkuranga

Na Mwandishi Wetu, Mkuranga
SERIKALI imepongezwa kwa kutambua juhudi zinazofanywa na wasanii, wanamichezo na waandishi wa habari za kujenga nyumba za makazi katika kijiji cha Mwanzega Mkuranga ambapo Mwenge wa Uhuru ulifika na kuweka jiwe la msingi Julai 22 mwaka huu.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Cassim Taalib katika risala aliyosoma mbele ya Kiongozi wa Mwenge kitaifa, Rachael Kassanda alisema Serikali kukitambua kijiji hicho kumeongeza ari ya wasanii kujenga nyumba za kisasa na kuongeza kasi ya maendeleo.

Alisema kijiji cha wasanii kimeanzishwa mahususi kwa ajili ya kuwakomboa na kuwapatia makazi ya kudumu wakisha staafu au kupotea kwa umaarufu wao katika fani zao.

Katika sherehe hizo ambazo wasanii zaidi ya 1,500 waliofurika kupokea mwenge wa uhuru kiongozi wa mbio za Mwenge, Rachael Kassanda aliwatoa wito kwa wasanii kuwa kioo halisi cha jamii kwa kuiga mema na kupiga vita mabaya katika jamii zinazowazunguka.

Awali Mkuu wa wilaya ya Mkuranga, Mercy Sila aliwaasa wasanii kutumia vipaji vyao kuwaelimisha jamii kuhusu maadili mema na kuiga yanayostahili kwa mila na desturi za Mtanzania.

Katika sherehe za kuweka jiwe la msingi zilizofanywa na kiongozi wa mbio za Mwenge,SHIWATA ilimsimika balozi wa kijiji hicho kuwa ni msanii maarufu na mtangazaji wa kituo cha Redio Times FM, Suzan Natasha ambaye aliahidi kukitangaza kijiji hicho katika mipaka ya ndani na nje ya Tanzania.

Sherehe hizo zilizoambatana na burudani mbalimbali zilizongozwa na Bendi ya Polisi, wanamuziki maarufu Kikumbi Mwanzo "King Kikii", Siza Mazongera "Wana Segere" na wasanii mbalimbali walitumbuiza.

Wengine walioshudia kuwekwa jiwe la msingi katika kijiji hicho baadhi yao ni wachezaji wa zamani wa Simba, Moses Mkandawile, George Lucas,Thom Kipese na kwa upande wa Yanga ni Abeid Mziba, Ramadhani Kampira, Bakari Malima, Omari Husein na wengineo.

Pia katika kusherekea mwenge wa uhuru SHIWATA ilitoa ofa bure kwa wanachama wapya kupimiwa viwanja vya kujenga nyumba bure katika kijiji hicho ambapo wanamichezo, wasanii na waandishi wa habari walipata fursa ya kuoneshwa viwanja watakavyotakiwa kujenga.

mwisho
Endelea Kusoma >>
0 comments

BREAKING NEWS : BASI LA HOOD LAPATA AJALI MBAYA ASUBUHI HII LIKITOKEA MBEYA

Muda mchache baada ajali kutokea 
 Askari wa usalama wa barabarani wakiwa wamefika eneo la tukio  na baadhi ya Mashuhuda wakishuhudia ajali hiyo

 Basi la Hood limepata ajali asubuhi hii likitoka Mbeya haijafahamika mara moja lilikuwa linaelekea wapi na haijafahamika kama kuna watu waliojeruhiwa, endelea kufutilia hapa kupata taarifa kamili hii ni taarifa ya awali.

Picha na Mbeya yetu Blog
Endelea Kusoma >>

Friday, July 25, 2014

MKUTANO KATI YA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM NA WANAMTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA NA TAMWA LEO

0 comments


 Usu Millya Mwanamtandao wa Ulingo wa Katiba na wanawake ambaye alikuwa ndiye mwezeshaji wa Mkutano huo ambao  ulikuwa ni wa siku mbili akiendelea kutoa mwongozo wa mkutano huo.
 Doreen E. Maro kutoka TAMPRODA ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba akiwakilisha Wafugaji Akileta Mrejesho wa walichokuwa wakikijadili katika Kundi lao juu ya mapendekezo ya kuimarisha Masuala muhimu ya Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya
 Dkt. Macca A. Mbalwa  Mkurugenzi wa Giyedo Tanzania akiwa anatoa Mrejesho wa kile ambacho walikuwa wamekijadili na kutoa mapendekezo yao ya Kuboresha masuala muhimu katika Rasimu ya pili ya Katiba Mpya.
 Salama Aboud Talib Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba  na Naibu Katibu Mkuu wa UWT akizungumzia makosa mbalimbali ambayo yapo katika Rasimu ya Pili ya Katiba mpya na kutoa mapendekezo kuwa Iboreshwe ili kuweka usawa.
 Executive Director wa  Women Fund Tanzania Mary Rusimbi akizungumza juu ya Majumuisho ya pomoja na Kupanga mikakati ambayo yatasaidia Kuimarisha Masuala Muhimu ya Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya
 Mgeni Hassan Juma Mwenyekiti wa Wawakilishi  Wanawake Zanzibar akitoa neno la Shukurani kwa wote waliohudhuria kwa muda wa siku mbili katika mkutano wa Wajumbe wa Bunge Maalum la  Katiba, Mtandao wa wanawake na TAMWA
 Profesa Ruth Meena  Akitoa Majumuisho pia kutoa Shukurani kwa wale wote waliohudhuria katika Mkutano huo uliochukua siku mbili.
 Valerie Msoka akifunga Rasmi Mkutano huo.
 Fredrick Msigala Mjumbe Bunge Maalum la Katiba ambaye ni Mlemavu wa Miguu akielezea masikitiko yake ya Jinsi watu wenye ulemavu wakiwemo wanawake na wanaume ambavyo wametengwa na kukosa haki zao, amesisitiza Serikali katika Rasimu Mpya ya Pili ya Katiba wawaangalie walemavu kwa umakini na ukaribu maana wanahaki sawa na watu wengine. Pia amesisitiza walemavu wajaliwe katika huduma za Afya mana ni Muhimu kwao. Mwisho amesisitiza kuwa wanawake wenye ulemavu wanahaki ya Kuolewa na kuto nyanyaswa pindi wanapokuwa katika ndoa zao.
 Modesta Mpereme ambaye ni Kiziwi hasikii lakini anaongea vizuri pia ni Mwenyekiti kutoka  Sauti ya Wanawake  wenye Ulemavu Tanzania, Ameiomba serikali iwe na vitendea kazi vya kutosha ambavyo vitawasaidia walemavu katika secta mbalimbali Mfano katika Mabenki kuwe na vifaa maalum vya kuwasaidia walemavu, Katika Upande wa Afya amesisitiza kuwe na hata watu wanaoweza kutoa msaada wa kutafsiri mambo mbalimbali mfano kwa Viziwi, wasio ona na ambao Hawawezi kuongea.
 Siti Ally Mwanasheria na Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba kutoka Zanzibar akisisitiza umuhimu wa usawa kati ya haki za wanawake na wanaume katika jamii , Pia alisisitiza juu ya mabinti wanaopata Mimba za utotoni wakiwa mashuleni na kusisitiza kuwa wanaruhusiwa kusimama masomo mpaka kipindi mtoto atakapokuwa mkubwa anaruhusiwa kuendelea na masomo,  Mwanaume aliyesababisha Mimba anaweza akashtakiwa .
 Baadhi ya Wajumbe wa Bunge Maalum la katiba pamoja na Wadau mbalimbali waliofika katika Mkutano huo.
Kawaida
Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu